Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii

KATIKA kuhakikisha nchi inaondokana na Maambukizo mapya ya ukimwi kwa vijana wadogo,Tume ya kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Imepanga kuwakutanisha wadau mbali mbali nchini kwa lengo kuwasaidia wasichana Balehe ili waweze kujitambua na kujiepusha makundi hatarishi.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Uhamishaji na Habari kutoka (TACAIDS) Jummanne Isango wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelezea kongamano la mwaka la wadau wanaotekeleza Afua za kusaidia mabinti wenye Rika Balehe na wanawake vijana.

Isango amesea amesema lengo la mkutano huo imetokana wasichana balehe na wanawake vijana wamekuwa wahanga wakubwa wa athari zinatokana na mdororo wa kijamii na kiuchumi ambazo husababisha kujiingiza katika vitendo vinavyoweza kuhatarisha masuala ya afya.

Hata hivyo.Isango amesema Mkutano huo unaopangwa kufanyika Tarehe 16 April hadi aprili tarehe 17 mwaka huu utafanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mwalimu nyerere (JNICC) jijini Dar es Saalam utajikita kutoa elimu kwa makundi hayo kuwapa utayari wa kupambana na changamoto husika,

Amesema mkutano nl huo ni wa mara ya kwanza kufanyika nchini unatajwa kuwakutanisha wadau mbali mbali wa maendeleo pamoja na asasi za kiraia wanaotekeleza afua mbali mbali za kuwasaidia wasichana hao.
Mkurugenzi wa Uhamasishaji na Habari wa Tacaids Jumanne Isango akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mkutano wa wadau wa kujadili masuala ya Ukimwi kwa Vijana utaofanyika kesho jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...