MEYA wa Temeke mkoani Dar es Salaam Abdallah Chaurembo amewataka wazazi kote nchini kuhakikisha wanawapatia huduma watoto walioko makambini na wale wa majumbani ili nao wajisikie kama vile wazazi wao wapo nao pamoja.

Rai hiyo ameitoa jana alipokuwa akizungumza na wazazi na wanafunzi wa shule ya secondari ya Joyland iliyoko kigamboni katika hafla ya kuchangia maendeleo ya watoto yatima katika shule hiyo. 

Alisema kuwa watoto yatima wamekuwa wakijisikia vibaya kutokana na wazazi walio wengi kuwatenga.

Hivyo Chaurembo amewataka wazazi kujitathimini juu ya jambo hilo kwani manyanyaso kwa yatima yamekuwa makubwa kutokana na sababu mbalimbali.

"Wazazi wezangu tujitolee ili kuwasaidia watoto yatima kote nchini ili nao wajisikie kama vile wazazi wao wapo hai hapa duniani, hata vitabu vya Mungu vinaimiza upendo kwa watoto hawa".alisema Chaurembo. 

Aidha meya huyo alifanikisha kupatikana kwa mamilioni ya fedha katika harambee hiyo ya kuwasaidia watoto yatima katika kituo hicho huku yeye akitoa milioni moja.

 Meya wa manispaa ya Temeke Mhe. Abdallah Chaurembo akizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi katika shule ya sekondari ya Joyland iliyopo kigamboni,kwenye hafla ya kuchangia watoto yatima leo jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa shule ya sekondari ya Joyland,Fredrick Okuku akizungumza machache katika hafla ya kuchangia watoto yatima  leo jijini Dar es Salaam.
 Picha ya pamoja,

 Wasanii wa  mbalimbali wa Bongo Fleva wakitoa burudani.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)

Wasanii wa  mbalimbali wa Bongo Fleva wakitoa burudani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...