Viongozi, Wafanyakazi na Wanachama wa Shirika la Under The Same Sun wakiwa katika picha ya Pamoja bungeni Jijini Dodoma leo.
  Viongozi, Wafanyakazi na Wanachama wa Shirika la Under The Same Sun wakiwa ndani ya Ukumbi  Bunge Jijini Dodoma leo.
  Viongozi, Wafanyakazi na Wanachama wa Shirika la Under The Same Sun wakiwa ndani ya Ukumbi  Bunge Jijini Dodoma leo.
Shirika la Under The Same Sun lenye kuhudumia na kutetea maslahi ya watu wenye ualbino nchini, linakusudia kufanya semina ya siku moja kwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania. 

Semina hiyo yenye lengo la kuwapatia uelewa kuhusu  ualbino, waheshimiwa wabunge inatarajiwa kufanyika jijini Dodoma kwenye Ukumbi wa Msekwa siku ja jumapili April 14. 

Under The Same Sun iliyoanzishwa miaka kumi iliyopita imekuwa ikitoa elimu kwa jamii juu ya ualbino na watu wenye ualbino kwa njia ya mikutano, semina na mafunzo mbalimbali pamoja na kutoa ufadhili wa elimu kwa watu wenye ualbino kuanzia ngazi ya awali, msingi, sekondari hadi chuo kikuu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...