*Azindua mabweni ya wanafunzi wenye ulemavu wa macho Tuangoma

* Aiagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi kwa tenda za miradi ya DMPD

Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam  Paul Makonda ameendelea na ziara yake ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika halmashauri ya Temeke ambapo amekagua ujenzi barabara ya Usalama Chang'ombe, ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika shule ya Sekondari kijichi mradi unaofadhiliwa na TAMISEMI, ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi wenye ulemavu wa macho ambapo pia ameweka jiwe la msingi, ujenzi wa mradi wa kisima cha maji katika kata ya Charambe pamoja na ujenzi wa kituo cha afya Yombo Vituka.

Akizungumza mara baada ya kufanya ziara hiyo Makonda ameipongeza halmashauri hiyo kwa kusimamia vyema miradi hiyo hasa ya barabara ambapo wameokoa gharama kubwa na kujenga barabara imara kwa milioni 900 kwa kilomita moja ukilinganisha na halmashauri ya Kinondoni inayojenga barabara ya kilomita moja kwa zaidi ya shilingi bilioni 2 ambapo amemuagiza Mkurugenzi wa TAKUKURU wa Mkoa huo kufanya uchunguzi wa utaratibu wa upatikanaji wa tenda kwenye miradi inayofadhiliwa na benki ya dunia (DMDP) baada ya kubaini matumizi mabaya ya fedha za serikali katika miradi hiyo kwa baadhi ya maeneo ya miradi.

Makonda amesema haiwezekani Kilomita Moja ya barabara ya Wilaya ya Kinondoni ikajengwa kwa Shilingi Billion 2.7 wakati kwa Wilaya ya Temeke barabara kama hiyo inajengwa kwa shilingi Milioni 900 pekee na yote inafadhiliwa na benki ya dunia.

Aidha  Makonda amesema kuwa wazawa wawe mstari wa mbele kuomba tenda za kusimamia miradi ya fedha nyingi ili kuweza kujitangaza na kuongeza ujuzi zaidi na sio kuyaachia makampuni makubwa pekee.

Vilevile Makonda ameipongeza halmashauri hiyo kwa kuwatazama watu wenye mahitaji maalumu kwa kujenga mabweni ya wanafunzi wenye ulemavu na amewataka kuwatazama watoto kutoka sehemu nyingine ili waweze kunufaika na fursa hiyo.

Ameeleza kuwa nafasi zitakazosalia katika bweni hilo wachukuliwe wanafunzi kutoka maeneo mengine kwa kuwa mradi huo ni wa pekee na maalumu katika mkoa huo na amezitaka halmashauri nyingine kuiga kutoka kwa wana Temeke. 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa, vyoo na mabweni katika shule ya msingi Tuangoma jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika shule ya sekondari Kijichi ambapo alizungumza na wanafunzi na kuwataka kuzingatia masomo na kuweka mbele nidhamu, jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Lusubilo Mwakabibi akizungumza na wanahabari mara baada ya zoezi la uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa madarasa, mabweni na vyoo katika shule ya msingi Tuangoma jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akitoa maelekezo mara baada ya kukagua ujenzi wa mabweni ya wanafunzi wenye ulemavu wa macho katika shule ya msingi Tuangoma, jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...