Baadhi ya wafanyabiashara waliopata fursa ya kuhudhuria maonyesho ya kibiashara yaliyoambatana na mafunzo ya uwekezaji katika sekta ya kilimo nchini China ambao waliwezeshwa safari yao na Benki ya CRDB kwa ushirikiano na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) wakiwa katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, jijini Dar es salaam walioporejea nchini baada ya kutembelea viwanda mbalimbali vya nchini China kwa mafunzo. Jumla ya wafanyabiasahara 60 kutoka maeneo mbalimbali nchini walihuhudhulia mafunzo hayo ya siku kumi (10) yatakayo wawezesha kutanua mtandao na kufungua soko jipya la kibiashara baina yao na wale wa kutoka China.
Mmoja wa viongozi wa safari hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA), Francis Lukwaro akizungumza na waandishi wa habari juu ya fursa za kibiashara walizoziona nchini China ambazo wameahidi kuzifanyia kazi hapa nchini.

Afisa Mahusiano wa Benki ya CRDB, Agnes Ngalo akizungumzia na waandhishi wa habari muda mfupi baada ya kurejea nchini wakitokea China, walikokwenda pamoja na wafanyabiasha hao kuhudhulia maonyesho ya kibiashara yaliyoambatana na mafunzo ya uwekezaji katika sekta ya kilimo nchini China ambao waliwezeshwa safari yao na Benki ya CRDB kwa ushirikiano na Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo (TCCIA) 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...