Na Karama Kenyunko, globu ya jami

WAFANYABASHRA wawili wakazi wa jijini Dar es Salaam, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na tuhuma za kula njama na kijipatia zaidi ya sh. Milioni 150 kwa njia ya udanganyifu .

Washtakiwa hao, Laurean Wambura (60) anaishi Mbezi Mshikamano na Allan Kwayu (25) wa Bunju Baharini wamesomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando.

Imedaiwa, katika siku tofauti tofauti kati ya Oktoba 2018 na Februari 2019, jijini Dar es Salaam, washtakiwa walitenda kosa la kujipatia RedHawks kwa njia ya udanganyifu.

Katika shtaka la pili, imedaiwa kati ya Januari 29 na February 27 mwaka huu, katika benki ya Exim tawi la Samora Avenue, washtakiwa kwa nia ya kudanganya au kutapeli, walijipatia USD 66,000 ambazo ni sawa na Sh. 150,678000  kutoka kwenye Akaunti ya Apollo international.  Kwa kudanganya kuwa wangewauzia copper Cathodes huku wakijua kuwa siyo kweli.

Hata hivyo, washtakiwa wako nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya mahakama yaliyowataka kuwa na wadhamini wawili kila mmoja na kuwasilisha hati ya Mali isiyohamishika yenye thamani ya nusu ya fedha wanazodaiwa kutapeli. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 2, mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...