Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Tasisi ya Pink Hijab Initiatives imeandaa mbio na Matembezi ya Kilometa kumi kuanzia Viwanja vya Green Ground Osterbay na kuishia katika Viwanja hivyo kwa kupitia barabara ya  Kenyata, Chole Road,Karume Road , Haile Salasi Road kupitia Coco Beach na kurudi katika Viwanjani hapo.

akizungumza na Globu ya Jamii Mratibu wa Mbio hizo kutoka Pink Hijab Initiative, Alhaj Jamal Mwarab Khalfan amesema kuwa lengo la mbio hizo ni kusaidia watoto waliopo katika Mazingira hatarishi katika Mkoa wa Tanga Wilaya ya Pangani.

"Sisi kama Tasisi ya Kislamu tumeona vyema kuitumia Ramdhani hii kama sehemu ya kurudisha tunachokipata kwa jamii kwa kuandaa mbio hizi na matembezi hili tuweze kuwasaidia watoto wetu waliopo katika Wilaya ya Pangani hivyo tunawaomba wote wenye mapenzi mema na watoto wetu kuja kujumuika na sisi April 21 Mwaka huu"amesema Alhaj Jamal.

Amesema mtu anayependa kushiriki mbio hizi anaweza kuchangia kiasi cha shilingi 20,000/-pia naweza kuwasiliana nasi kupitia namba 0713433407 au 0655445105 hili aweze kushiriki na kuchangia zaidi.

--

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...