Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Wito umetolewa kwa Wanawake wanaofanya shughuli za uvuvi na kuchakata mazao ya uvuvi kutumia chama chao kuweza kupanua fursa ya masoko baina ya wao kwa wao kutokana na sehemu wanazotoka.

Hayo yamesemwa leo April 15 jijini Dar es Salaam 2019 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama alipokuwa akifungua kikao cha kwanza cha TAWFA Kilichofanyika katika Hotel ya Mbezi Garden Jijini Dar es Salaam.

“TAWFA ni mtandao au chombo kitakachotumika kuwaunganisha kwa pamoja Wanawake wote wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi hapa nchini ,pia kupitia TAWFA,nataraji kwamba wanawake watatoa changamoto na uzoefu wao kwa sauti moja katika shughuli za uvuvi na kuuza mazao ya uvuvi”amesema Dk . Rashid.

Amesema kuwa TAWFA Ndio chombo pekee kutoka Tanzania kitakachokuwa mwanachama katika mtandao wa Africa (Africa Women fish processors and Traders Association-AWFISHNET) Ambao umeunganisha wanawake wote Africa wanaojishughulisha na uchakataji na biashara ya samaki na mazao yake ili wawe na sauti moja katika kushiriki kwenye masuala mbalimbali.

Pia alitoa wito kwa wanawake wote wanaohusika katika mtandao wa TAWFA waweze kushirikiana,kupendana na kusaidiana katika shughuli zenu ili kuwa na uelewano wa kibiashara na kukuza kipato na uchumi kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Chama cha Wanawake wanaojishughulisha na kuchakata mazo ya uvuvi nchini.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akizungumza na Wanachama wa Chama cha Wanawake wanaojishughulisha kuchakata mazo ya Uvuvi nchini(TAWFA) Wakati wa hafala ya ufunguzi wa Chama hicho Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Emedo akizungumza mbele ya mgeni rasmi kumeuleza mchakato wa kuanzishwa kwa TAWFA
Sehemu ya Wanachama wa TAWFA Walioshiriki uzinduzi wa chama chao jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akikagua baadhi ya mazo ya uvuvi yalionyeshwa na Wanawake hao.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akikagua baadhi ya mazo ya uvuvi yalionyeshwa na Wanawake hao.
Sehemu ya Wanachama wa TAWFA Walioshiriki uzinduzi wa chama chao jijini Dar es Salaam
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Dk .Rashid Tamatama akiwa katika picha ya pamoja na Wanachama wa TAWFA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...