Kiongozi wa wasanii wa kundi la uzalendo kwanza Steven Nyerere akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani leo jijini Dar es Salaam kuhusu  Wizara ya Utalii na bodi ya Utali kuendelea kuona mchango wa wasanii katika kuutangaza utalii. (Picha na Emmanuel Massaka,MMG).


*Lengo ni kujifunza,kuongeza pato la Taifa...Stive Nyerere asema Tanzania imebarikiwa

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

BAADA ya Tanzania kuwa ndio nchi ya kwanza duniani kuwa na vivutio vingi vya utalii, wasanii wa filamu na muziki wa dansi nchini, wanaounda kundi la wazalendo kwanza   wamewaomba wananchi  kutembelea vivutio hivyo kwa lengo la kujifunza na kukuza pato la Taifa

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kutangaza hifadhi mpya tatu za utalii nchini, uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Wazalendo Kwanza, Steven Nyerere amesema ni muhimu kwa watanzania kutembelea vivutio hivyo vya utalii kwani watapata fursa kujifunza, kuona mambo ya kale pamoja na wanyama mbalimbali. 

Ameongeza kwani hifadhi mbalimbali za taifa zinapoingiza watatilii kutoka ndani na nje ya nchi, fedha zinazopatikana zinatumika katika maendeleo mbali mbali ikiwamo ujenzi wa hospitali, shule, viwanja vya michezo pamoja na  miundombinu ya barabara.

Amesema Tanzania ni nchi ambayo imebarikiwa katika masuala ya utalii kitu ambacho kinasababisha kuwepo kwa watalii wengi wakiwemo Wazungu ambao wengi wao wamekuwa wakipishana angani kuja nchini.

" Mbuga hizi za wanyama na vivutio vingine vya utalii vinapoingiza watalii tunapata fedha ambazo zinatumika katika maendeleo mbalimbali kama ujenzi wa hospitali na viwanja vya michezo," amesema.

Amefafanua hifadhi hizo mpya tatu ambazo ni Biharamulo ,Burugi na Kimisi ni moja kati ya vivutio vipya vya utalii nchini ambavyo vitakuwa vikitangazwa na kundi hilo la Wazalendo kwanza kwa lengo la kuhamasisha jamii na watalii kutoka nje ya nchi kuja kutembelea.

"Kampeni hii ya kutangaza vivutio hivi vipya itakuwa na mabalozi wanne ambazo ndio watatumika kutangaza, Sisi wazalendo kwanza ambapo pamoja na mabalozi hao wapya tutafanya ziara kwenda kuvitembekea  vivutio hivyo na na tutafika mpaka Chato pia na kwa mara ya kwanza jambo hili litakuwa na mvuto wa pekee," amesema.

Kwa upande wake Balozi wa Utalii nchini Nangasu Warema amesema vivutio hivyo vipya vitatangazwa ili kila mtanzania aweze kuvifahamu na kupata fursa ya kuvitembelea.

"Tumezindua rasmi kampeni ya kutangaza hifadhi hizi mpya ya Biharamulo, Burugi na Kibisi, tunawaomba wawekezaji waje kuwekeza kwa wingi katika hifadhi hizi kwani jambo hili lazima litawalipa tu," amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...