Wataalamu 25 wa Ulinzi na Usalama wa vyanzo vya mionzi kutoka katika nchi sita za Afrika wanaoshiriki katika mafunzo ya wiki mbili ya jinsi ya kuendesha mafunzo ya ulinzi na usalama wa vyanzo vya mionz katika nchi zao wakiwa katika picha ya pamoja katika Makao Makuu ya Ofisi ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) Jijini Arusha. Mafunzo hayo yanaendeshwa na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania kwa ushirikiano na Jumuia ya Umoja wa Ulaya (EU).
Wataalamu wa Ulinzi na Usalama wa vyanzo vya mionzi kutoka katika nchi sita za Afrika wanashiriki katika mafunzo ya wiki mbili ya utoaji mafunzo ya ulinzi na usalama wa vyanzo vya mionzi yanaoendeshwa na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania (TAEC) kwa ushirikiano na Jumuia ya Umoja wa Ulaya (EU)
Mkuu
wa Kitengo cha mawasiliano cha Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania Peter
Ngamilo amesema kuwa mafunzo hayo yanafanyika katika ofisi za Tume ya
Nguvu za Atomiki Tanzania jijini Arusha na jumla ya washiriki 25
wanashiriki mafunzo hayo kwa kwa lengo la kupata ujuzi wa namna ya
kufundisha wataalamu mbali mbali wanaohusika na ulinzi na usalama wa
vyanzo vya mionzi katika nchi zao.
Ngamilo
amesema kuwa baada ya wakufunzi hao wa ulinzi na usalama wa vyanzo vya
mionzi kumaliza mafunzo yao watakuwa na uwezo wa kutoa mafunzo kwa
wafanyakazi wenzao wa idara mbalimbali za kitaifa katika nchi zao katika
kuhakikisha kuwa vyanzo vya mionzi vinatumika katika njia zilizo salama
na halali.
“Wakufunzi
hawa waliopo kwenye mafunzo wakitoka hapa watakuwa na uwezo wa kuandaa
na kufanya mafunzo ya ulinzi na usalama wa vyanzo vya mionzi kwa wadau
mbalimbali katika nchi zao, pia watatumika kama wataalamu katika
kushughulikia matukio yoyote ya maafa ya vyanzo vya mionzi iwapo
yatatokea katika nchi za bara la Afrika”alisema Ngamilo.
Hata
hivyo amesema kuwa vyanzo vya mionzi visipodhibitiwa vinaweza kutumika
katika vitendo vya kigaidi na kuleta madhara makubwa kwa jamii na
kuathiri shughuli za kimaendeleo na kiuchumi
Na
pia amesema kuwa wakufunzi hao wanajengewa uwezo wa kutoa mafunzo ya
kubaini usafirishaji haramu wa vyanzo vya mionzi hasa kwa wataalamu wa
mamlaka za ulinzi na usalama ikiwemo Polisi, Walinzi waliopo mipakani na
wasimamizi wa Tekinolojia ya Nyuklia, maafisa forodha na wataalamu wa
kupambana na majanga ya nyuklia.
Amezitaja
metaja nchi wanazotoka washiriki wa mafunzo hayo ni pamoja na Burundi,
Uganda, Congo(DRC), Zambia,Ghana na wenyeji Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...