Na.Khadija seif,Globu ya jamii

HATIMAE washindi 15 wa wiki ya saba ya promosheni ya “Tia kitu pata vituz” inayoendeshwa na Kampuni ya MultiChoice Tanzania watangazwa rasmi.

Afisa Mwandamizi wa bodi ya michezo ya michezo ya kubahatisha Bw. Jehud Ngolo amesema Kampeni hiyo ni ya kipindi cha wiki 8, ambapo washindi 15 hutangazwa kila wiki hivyo jumla ya washindi 120 katika kipindi chote cha promosheni hiyo.

Afisa Uhusiano wa Kampuni ya MultiChoice Tanzania Grace Mgaya wakati wa kufanya droo ya wiki ya saba ya promosheni hiyo amesema promosheni hiyo ni wazi kuwa inawalenga wateja wote wa DStv ambao watalipia vifurushi vyao kabla havijakatika. 

“Mteja yeyote wa DStv atakayelipia kifurushi chake kabla hakijakatika moja kwa moja anaingia katika droo na ana fursa ya kujishindia kifurushi chake kwa muda wa miezi miwili mfulilizo” alisema Mgaya.


Akizumgumza baada ya kupatiwa taarifa kuhusu ushindi wake huo Angelina Michael  ambaye ni mteja wa DStv aliyepo mkoani Arusha amesema kuwa anafurahishwa na jitihada zinazofanywa na DStv siku hadi siku katika kuwajali na kuhakikisha wateja wake wanapata huduma zilizo na ubora wa hali ya juu. 
.
Huku Deus Nyakriga kutoka mkoani Mara, ameishukuru sana DStv kwa zawadi hiyo na kueleza kuwa licha ya kuwapatia huduma nzuri DStv inawajali sana wateja wake. 

Pia amewapa ujasiri wateja wengine wa DStv kulipa kwa wakati ili kujipatia nafasi hiyo ya kuingia kwenye droo hiyo ya kushinda miezi miwili bila malipo.
Afisa Uhusiano MultiChoice Tanzania Grace Mgaya {katikati} Akizungumza kwa simu na moja ya washindi wa promosheni hiyo. Kulia ni Afisa wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Jehud Ngolo na kushoto ni Benson Urio wa Kitengo cha Teknohama. Promosheni hiyo ni kwa wateja wanaolipia kwa
wakati kabla vifurushi vyao havijakatika hivyo kupata fursa ya kushinda kifurushi cha miezi miwili. Promosheni hii itaendelea kwa kipindi cha wiki 5 zijazo ambapo jumla ya washindi 120 
watapatikan 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...