Na.Paschal Dotto-MAELEZO.

Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji, Angellah Kairuki ameanza kukutana na wawekezaji kutoka balozi za Ufaransa, Uholonzi, Norway na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Marekani, USAID, mazungumzo mafupi baina wao yamefanyika leo kwa wakati tafaouti, huku Waziri Kairuki akisema kuwa mazungumzo hayo yalilenga kuongeza ushirikiano katika sekta ya uwekezaji nchini.

Katika mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini, Frederic Clavier, Waziri Kairuki alisema kuwa nchi ya ufaransa na Tanzania zina ushirikiano wa muda mrefu katika sekta mbalimbali ikiwemo ya uwekezaji pamoja na biashara.

“tulikuwa na mazungumzo na Balozi wa Ufaransa ambaye tumejadili mambo mbalimbali katika ushirikiano wetu, ili kuwaita wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Ufaransa waje nchini kama ilivyokuwa mwaka jana,” alisema Waziri

Akitoa mfano Waziri Kairuki alisema kulikuwa na ugeni wa wawekezaji na wafanyabiashara kutoka huko Ufaransa na walifanya majadiliano na Tasisi ya uwekezaji nchini, TPSF, akasema, “kwa hiyo na mwaka huu tumekubaliana watawaalika tena TPSF na TIC (Kituo cha uwekezaji) ili kuweza kujadili mambo ya uwekezaji”.

Kukutana na wawekezaji hao kutoka nchi mbalimbali Waziri Kairuki amesema kutabainisha fursa kadhaa na kufuatilia changamoto ili uwekezaji mkubwa uweze kufanyika nchini, pia Waziri Kairuki alieleza kuwa wamekubaliana na Balozi wa Ufaransa kuwa na ugeni mkubwa wa wawekezaji kati ya mwezi Mei na Septemba ambao watakuja kuwekeza katika sekta ya kilimo.

Aidha, Waziri Kairuki alimhakikishia Balozi wa Ufaransa kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa wawekezaji kwa kuendelea kuwajengea mazingira na hivyo kuhimiza wawekezaji kutoka Ufaransa kuongezaka nchini kutoka 40 waliowekeza kwa sasa.

“Uwekezaji unaongeza pato letu, unaongeza fedha za kigeni, ajira pamoja na masuala mengine katika uchumi, katika hili Ufaransa wamesema wako tayari kuanzisha jukwaa la biashara kwa wafanyabiashara kutoka Tanzania na Ufaransa ili kuweza kuvutia zaidi wawekezaji”, Waziri Kairuki.

Aidha, Balozi Clavier aliongeza kuwa Serikali ya Ufaransa inaridhishwa na jitihada za Rais Magufuli na kuwa nchi yake ilikuwa inachangia maendeleo ya nchi Euro milioni 50 kwa mwaka na imeongeza mpaka kufika Euro milioni 100, ambazo zitatumika katika uwekezaji mbalimbali hapa nchini ikiwemo Sekta ya mafuta, Viwanda vya Dawa na kilimo.

Katika mazungumzo mengine na Mabalozi wa Uholanzi, Jeroen Verheul, Norway, Elisabeth Jacobsen pamoja na Mkurugenzi Mkazi USAID, Andy Karas, Waziri Kairuki amewahakikishia kuwa atakutana na wawekezaji kutoka nchi hizo, kuwasikiliza changamoto zao na kuzitatua ili kuimarisha sekta ya uwekezaji nchini.
Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu, Angellah Kairuki akifafanua jambo kuhusu sekta ya uwekezaji nchini kwa Balozi wa Norway nchini, Elisabath Jacobsen walipokuatana leo Ofisini Kwakwe Jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...