Katibu mkuu wizara ya kilimo mhandisi mathew mtigumwe amekitaka kikosi kazi kinachojihusisha na uandaaji wa mpango mkakati wa kuendeleza uzalishaji wa zao la mpunga nchini kuhakikisha kinaanda rasimu itakayowezesha uzalishaji wa zao hilo kukuwa mara mbili zaidi kutoka tani milioni 2.2 hadi kufikia tani 4.5 ifikapo 2030.
Akizungumza na wataalam hao na wadau kutoka taasisi binafsi katika katibu mkuu mtigumwe amesema kufuatia wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuanzisha mpango mkakati wa kuendeleza zao la mpunga yaani national rice development strategy (nrsd) 1 mwaka 2008 kuwa na matokeo chanya ya kuongeza uzalishaji wa mpunga kutoka tani laki  899,000 hadi kufikia tani milioni 2.2 mwaka 2018 ambapo ili kukuza zaidi uzalishaji imeanzishwa nrds 2 itakayokwenda mpaka mwaka 2030 huku lengo likiwa ni kufikia tani za mpunga milioni 4.5…
"Mpango huu utatekelezwa kwa muda was miaka 12 kuanzia mwaka 2018 had I mwaka 2030 na tayari maandalizi Yake yalianza mwaka 2018 kwa kuanzia kuainishwa takwimu zinazohitajika" amesema mtigumwe.
Mwenyekiti wa kikosi kazi hicho  joseph lubiloh, amesema kuwa matarajio waliyonayo mara baada ya kukamilika kwa mpango wa awamu ya pili na hadi sasa kikosi hicho kimefanikisha kukusanya takwimu kamili za kufanikisha mpango huo huku wadau wengine wakifafanua mipango iliyopo katika kufanikisha mpango huo kuwa ni kushirikiana na serikali kukamilisha juhudi hizo.
 Katibu mkuu wizara ya kilimo mhandisi mathew mtigumwe akizungumza jambo na wanakikosi kazi pamoja na wadau mbalimbali.
 kikosi kazi kinachojihusisha na uandaaji wa mpango mkakati wa kuendeleza uzalishaji wa zao la mpunga nchini pamoja na Katibu mkuu wizara ya kilimo mhandisi mathew mtigumwe aliyekaa katikati
 wadau mbalimbali na kikosi kazi kinachojihusisha na uandaaji wa mpango mkakati wa kuendeleza uzalishaji wa zao la mpunga nchini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...