Katibu mkuu wizara ya
kilimo mhandisi mathew mtigumwe amekitaka kikosi kazi kinachojihusisha na
uandaaji wa mpango mkakati wa kuendeleza uzalishaji wa zao la mpunga nchini
kuhakikisha kinaanda rasimu itakayowezesha uzalishaji wa zao hilo kukuwa mara
mbili zaidi kutoka tani milioni 2.2 hadi kufikia tani 4.5 ifikapo 2030.
Akizungumza na
wataalam hao na wadau kutoka taasisi binafsi katika katibu mkuu mtigumwe
amesema kufuatia wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuanzisha mpango
mkakati wa kuendeleza zao la mpunga yaani national rice development strategy
(nrsd) 1 mwaka 2008 kuwa na matokeo chanya ya kuongeza uzalishaji wa mpunga
kutoka tani laki 899,000 hadi kufikia
tani milioni 2.2 mwaka 2018 ambapo ili kukuza zaidi uzalishaji imeanzishwa nrds
2 itakayokwenda mpaka mwaka 2030 huku lengo likiwa ni kufikia tani za mpunga
milioni 4.5…
"Mpango
huu utatekelezwa kwa muda was miaka 12 kuanzia mwaka 2018 had I mwaka
2030 na tayari maandalizi Yake yalianza mwaka 2018 kwa kuanzia
kuainishwa takwimu zinazohitajika" amesema mtigumwe.
Mwenyekiti wa kikosi kazi hicho joseph lubiloh, amesema kuwa matarajio waliyonayo mara baada ya kukamilika kwa
mpango wa awamu ya pili na hadi sasa kikosi hicho kimefanikisha kukusanya
takwimu kamili za kufanikisha mpango huo huku wadau wengine wakifafanua mipango
iliyopo katika kufanikisha mpango huo kuwa ni kushirikiana na serikali kukamilisha juhudi hizo.
Katibu mkuu wizara ya kilimo mhandisi mathew mtigumwe akizungumza jambo na wanakikosi kazi pamoja na wadau mbalimbali.
kikosi
kazi kinachojihusisha na uandaaji wa mpango mkakati wa kuendeleza
uzalishaji wa zao la mpunga nchini pamoja na Katibu mkuu wizara ya
kilimo mhandisi mathew mtigumwe aliyekaa katikati
wadau mbalimbali na kikosi kazi kinachojihusisha na uandaaji wa mpango mkakati wa kuendeleza uzalishaji wa zao la mpunga nchini
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...