Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akisisitiza umuhimu wa waandishi wa Habari kuzingatia maadili katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku ili kulinda tunu za Taifa leo Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Juliana Shonza akijibu hoja za wabunge wakati wa kuhitimisha  mjadala wa hoja zilizotolewa kwa wabunge wakati wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim  Majaliwa akimpongeza Waziri wa  Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe na Naibu Waziri wake  Juliana Shonza mara baada ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara hiyo leo Bungeni Jijini Dodoma.
 Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali  Dkt. Hassan Abbasi akifurahia jambo na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe.
Watendaji wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wakiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi Susan Mlawi wakifuatilia majadiliano ndani ya ukumbi wa ubunge leo kabla ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2019/2020.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji wa Wizara  mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara hiyo leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola akisisitiza kuhusu hatua zinazochukuliwa na Serikali kushughulikia makosa ya jinai ikiwemo kufanya  uchunguzi dhidi tuhuma husika na kubaini ukweli.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango akisisitiza kuhusu utaratibu unaotumiwa na Shirika la Fedha Duniani kutoa taarifa ya hali ya uchumi kwa nchi wananchama Leo Bungeni Jijini Dodoma.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akisisitiza jambo kwa sehemu ya wasanii leo Bungeni Jijini Dodoma.
 Mmoja wa wasanii akimpongeza Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe  mara baada ya kupitishwa kwa bajeti ya Wizara hiyo leo Jijini Dodoma. (Picha zote na Frank  Mvungi- MAELEZO, Dodoma)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...