Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) itaendesha kambi kwa ajili ya upasuaji wa matundu madogo (Endoscopic Surgery) kuanzia tarehe 7 mpaka 21 mwezi Juni, 2019.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya kinamama na uzazi katika Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH), Dkt. Januarius Hinju, anasema kambi hiyo ya wiki mbili itaendeshwa kwa ushiriano kati ya madaktari bingwa wa BMH na wenzao kutoka Marekani.

“Tunawakaribisha watanzania na hasa wakazi wa Dodoma na mikoa ya jirani wenye matatizo ya uzazi, kutokushika mimba, ngiri (hernia) waje BMH kuanzia sasa kwa ajili ya uchunguzi ili watakaokutwa na matatizo wapangiwe huduma hiyo ya upasuaji wakati wa kambi hiyo,” anasema Dkt Hinju, ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji wa BMH.

Dkt. Hinju anasema upasuaji wa matundu madogo ni upasuaji wa kisasa ambao una faida kubwa kwa mgonjwa kulinganisha na upasuaji wa kawaida. 

Alitaja baadhi ya faida hizo kuwa ni pamoja na muda mchache anaotumia mgonjwa kupona baada ya upasuaji, maumivu kidogo pamoja na mgonjwa kutokutokwa na damu nyingi wakati wa upasuaji. 

BMH inaendesha kambi hii yenye lengo la kuimarisha huduma za kibingwa kwa mwaka wa pili mfululizo katika Hospitali hiyo. Kambi ya kwanza ilifanyika Julai mwaka jana.

Imetolewa na Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano
Hospitali ya Benjamin Mkapa
 Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Akinamama Wakifanya Upasuaji wa Kutumia Matundu Madogo (Endoscopic Surgery)  Katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Hivi Karibuni.


Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Akinamama Wakifanya Upasuaji wa Kutumia Matundu Madogo (Endoscopic Surgery)  Katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Hivi Karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...