Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (wapili kushoto), akiongozwa na
Mhandisi Msimamizi wa Ujenzi wa jengo la kiwanja cha ndege Terminal III, Barton
Komba, wakati alipofanya ukaguzi wa kuona maendeleo ya mradi huo ambao hadi
sasa umekamilika kwa asilimia 99.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akitoka kukagua maendeleo ya
mradi wa ujenzi wa kiwanja cha ndege terminal III jijini Dar es salaam, ambapo
IGP Sirro alisema Jeshi la Polisi limejipanga kuimarisha usalama kiwanjani hapo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro, akikagua gwaride aliloandaliwa
kwa ajili yake wakati alipofanya ziara ya ukaguzi katika Kikosi cha Kutuliza Ghasia
FFU Ukonga Dar es salaam, ambapo katika ukaguzi wake IGP Sirro alizungumza na
maofisa na askari wa kikosi hicho.
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Simon Sirro (katikati) akitoa maelekezo kwa
maofisa wa Jeshi hilo wakati alipofanya ziara ya ukaguzi katika Kikosi cha Kutuliza
Ghasia FFU Ukonga Dar es salaam, kulia ni kamishna wa Operesheni na Mafunzo
CP Liberatus Sabas. Picha na Jeshi la Polisi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...