Na Agness Francis, Michuzi Tv.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Kidao Wilfred pamoja na Mkurugenzi wa Mashindano TFF Salum Madadi wanatakiwa kushiriki kwenye semina ya FIFA ya siku mbili huko nchini Malawi.
Uongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) umetanabaisha kuwa semina hiyo itakayofanyika Blantyre nchini humo ambayo inatarajia kuanza leo Mei 15 na kumalizika kesho Mei 16 mwaka huu itahusiana na miundo mbinu
Uongozi huo umesema kuwa Washiriki 34 kutoka nchi mbalimbali watashiriki katika semina hiyo inayosimamiwa na FIFA, huku ajenda kubwa ikiwa ni masuala ya miundo mbinu ya uboreshaji wa viwanja vya mpira wa miguu.
Mbali na Tanzania tu nchi nyingine kutoka barani Afrika zimealikwa kuhudhuria mkutano huo wa FIFA.
"Nchi hizo ambazo ni Uganda,Seychelles,Sudan Kusini,Misri,Eswatini,Eritrea, Gambia,Lesotho,Cape Verde,Liberia,Msumbiji, Somalia,Afrika Kusini na Wenyeji wao Malawi" umesema uongozi wa TFF.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Kidao Wilfred pamoja na Mkurugenzi wa Mashindano TFF Salum Madadi wanatakiwa kushiriki kwenye semina ya FIFA ya siku mbili huko nchini Malawi.
Uongozi wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) umetanabaisha kuwa semina hiyo itakayofanyika Blantyre nchini humo ambayo inatarajia kuanza leo Mei 15 na kumalizika kesho Mei 16 mwaka huu itahusiana na miundo mbinu
Uongozi huo umesema kuwa Washiriki 34 kutoka nchi mbalimbali watashiriki katika semina hiyo inayosimamiwa na FIFA, huku ajenda kubwa ikiwa ni masuala ya miundo mbinu ya uboreshaji wa viwanja vya mpira wa miguu.
Mbali na Tanzania tu nchi nyingine kutoka barani Afrika zimealikwa kuhudhuria mkutano huo wa FIFA.
"Nchi hizo ambazo ni Uganda,Seychelles,Sudan Kusini,Misri,Eswatini,Eritrea,
Mtendaji mkuu wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Wilfred Kidao.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...