Na Ripota Wetu

KIONGOZI wa Baraza la Wawakilishi nchini Uingereza Andrea Leadsom amejiuzulu kwa madai kuwa hana imani na tena na njia anayotumia Waziri Mkuu Theresa May kama inaweza kuufanikisha mchakato wa Uingereza kujitoa Umoja wa Ulaya ama Brexit.

Hatua hiyo inaongeza shinikizo kwa Waziri Mkuu May ambapo Leadsom anayetambulika zaidi kwa kuunga mkono Brexit amemuandikia barua May akimtolea mwito wa kuchukua uamuzi sahihi kwa ajili ya maslahi ya taifa, serikali na chama chao.

Kwa mujibu wa mtandao wa DW -Swahili ni kwamba kujiuzulu kwake kunakuja siku moja kabla ya Uingereza kushiriki uchaguzi wa Bunge la Ulaya.

Wakati hayo yakiendelea  May hapo jana aliendelea kupuuza ongezeko la miito ya kumtaka ajiuzulu, licha ya kuongezeka kwa upinzani kutoka kwa wabunge na mawaziri wa chama chake cha Conservative kuhusu mpango wake wa karibuni wa Brexit.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...