Kampuni maarufu ya kimataifa ya mauzo ya moja kwa moja yenye asili ya Asia, QNET imeendesha kongamano la siku tano la kimataifa ambalo linaleta pamoja takribani wajasiriamali 13,000 kutoka maeneo mbalimbali duniani katika kisiwa cha Penang, Malaysia Takribani wajasiriamali wa kiafrika wenye shauku wapatao 2600  walishiriki katika kongamano la mwaka huu.

Kongamano ambalo hufanywa mara mbili kwa mwaka la (V-Convention) ni tukio la kipekee ambalo huleta pamoja wateja na wasambazaji wa QNET kutoka maeneo mbalimbali duniani, washirika wake wa kibiashara, na pia maofisa wa serikali kuja kujionea bidhaa na huduma za QNET na kuelewa vyema biashara yake. 

Kongamano la siku tano ilijumuisha mfululizo wa programu za mafunzo, hotuba za uhamasishaji, kutambulisha bidhaa mpya za mtindo wa maisha wa QNET na matukio ya burudani. Kivutio kikubwa mwaka huu ni QNET Carnival ambayo ilionyesha zaidi ya nembo au lebo 30 za bidhaa za QNET katika moja ya maonyesho makubwa kuwahi kufanywa na kampuni hiyo. Bidhaa mpya zilizozinduliwa mwaka huu ni pamoja na virutubisho vipya kwaajili ya afya ya wanaume vinavyoitwa QAlive, na toleo lenye ukomo la saa za kifahari kwaajili ya kumbukizi ya miaka mitano ya ushirikiano kati ya QNET na klabu ya mpira wa miguu ya jiji la Manchester  (Manchester City Football Club). Moja kati ya dondoo zilizoshika hisia za watu ni sherehe za mahafali ya wateja ambao wamekamilisha kozi zao kwa njia ya mtandao kupitia qLean, bidhaa ya elimu ya QNET, ambayo ni maarufu sana miongoni mwa wateja katika kanda ya Sahara ya Afrika. 

Washiriki vile vile walipewa fursa ya kusikiliza kutoka kwa wazungumzaji rasmi ambao wameshinda vikwazo vikubwa na kufanikisha ndoto zao.  Farouk Saad Hamad Al-Zuman, raia wa kwanza wa Saudi Arabia kupanda mlima Everest, na Sparsh Shah, mvulana mwenye umri wa miaka 15 raia wa marekani mwenye asili ya India aliyezaliwa na tatizo la mifupa dhaifu (brittle bones), ambaye alipewa siku 2 za kuishi na madaktari baada ya kuzaliwa, na sasa ni nyota katika mtandao wa Youtube kwa mtindo wake wa kipekee wa mziki ambao anaunganisha pamoja muziki wa classical na rap.  

Bwana Koné Doupin, Mwakilishi wa Kujitegemea anayeshiriki katika kongamano hilo la (V-Convention) kutokea Ivory Coast alisema:  "Nina furaha sana kuwa hapa mwaka huu.  Tangu nilipojiunga na QNET miaka kumi iliyopita, sijawahi kukosa kongamano la -V lolote kwa sababu ni fursa ya kipekee kukutana na viongozi wetu wa juu, kujifunza kutoka kwao, kukutana na watu kutoka sehemu mbalimbali na kugundua upekee wa bidhaa mpya.  Nina shauku kubwa ya kujaribu bidhaa mpya ya QAlive, kirutubisho kipya cha wanaume na kugundua ni jinsi gani kinaweza kuboresha maisha yangu."

Sherehe za ufunguzi ziliongozwa na watu mbalimbali maarufu kutoka Malayasia na Asia ya Kusini Mashariki.  Mgeni rasmi kutoka Afrika, Bwana Cissé Ibrahim Sory vile vile alikuwepo katika sherehe za ufunguzi, Bwana Cissé Ibrahim Sory ni Mjumbe wa Baraza la Mawaziri kutoka ofisi ya Rais katika Jamhuri ya Guinea-Conakry.

Afisa Mtendaji Mkuu mpya wa QNET aliyeteuliwa, Bi. Malou Caluza alisema: "Matukio kama haya ya Kongamano (V-Convention) hutupa fursa ya kuwahudumia wasambazaji wetu na kuwapa fursa ya kuona na kushuhudia mtindo wa Kuishi Kikamilifu (Absolute Living) ambao inaongoza biashara yetu, Vile vile ni jukwaa bora la kusherehekea ari ya ujasiriamali ambayo kampuni ya mauzo ya moja kwa moja kama QNET inachochea kwa mamilioni ya watu duniani kote, kuwasaidia kuboresha maisha yao na kuchangia katika jamii."

Akiongeza katika hilo, Meneja Mkuu wa QNET wa kanda ya Kusini mwa Jangwa la Sahara Bwana Biram Fall, alisema: "V-Malayasia inafuata msimu wa kongamano la QNET Expo wa mwaka 2019 wenye mafanikio wenye jina la Kuisi Kikamilifu (Absolute Living), linaloenda sambamba na kanuni ya kampuni ya mauzo ya moja kwa moja QNET na falsafa yake ya  RYTHM - Jiinue Uweze Kuwasaidia Wanadamu (Raise Yourself to Help Mankind) Kongamano la mwaka 2019 lilianzia jijini Dar es salaam, Tanzania mwezi uliopita, kisha likahalia Kumasi, Ghana na sasa nchini Malayasia kwaajili ya kongamano la kiulimwengu la V-Convention.  Baadae nchi zingine za Afrika zitakuwa wenyeji wa kongamano la Kuishi Kikamilifu (Absolute living expo)."

QNET, inauza reja reja bidhaa mbalimbali za Afya na ustawi, huduma binafsi na urembo, sikukuu, utunzaji wa nyumba na kozi kwa njia ya mtandao miongoni mwa nyingi zingine ambazo zinaboresha maisha ya kila siku ya wateja wake duniani kote. QNET iliwekwa katika moja kati ya makampuni 100 makubwa na imara ya MLM  (Solid Top MLM Companies) kwa mwaka 2018 na Portal ya habari za mauzo ya moja kwa moja ya Business for Home.

Katika Afrika Magharibi, Chama cha Ghana cha CSR (GHACEA) mwaka 2018 kiliitunukia QNET kuwa Kampuni ya Mwaka ya Biashara ya Mtandao (E-Commerce Company of the Year.)
 Afisa Mtendaji Mkuu wa QNET,  Ms. Malou Calouza(wa kwanza kushoto)  na Maofisa wa serikali ya Malaysia wakikata  utepe kuzindua rasmi kongamano la V-Convetion lililofanyika mjini Penang, Malaysia hivi karibuni. Wengine ni wajumbe wa Bodi wa QNET.
Meneja wa QNET wa kusini mwa Afrika, Biram Fall (kushoto)akiwa amepozi na Mjumbe wa Baraza la Mawaziri Ofisi ya Rais, Guinea-Conakry, Ndugu Cissé Ibrahim Sory wakati wa kongamano la QNET la V-Convetion lililofanyika mjini Penang, Malaysia hivi karibuni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...