Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki akizungumza wakati wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na wawekezaji kutoka Jimbo la Zhejiang la China lililofanyika jijini Arusha tarehe 13 Mei 2019. Katika hotuba yake Mhe. Kairuki alisisitiz akuwa Tanzania ni eneo salama zaidi kuwekeza barani Afrika kutokana na sababu za msingi kama amani, mazingira na sheria rafiki za uwekezaji pamoja na maeneo lukuki ya kuwekeza kama kilimo, madini, usindikaji, viwanda na utalii. Kongamano hilo ambalo lilihudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka Serikalini na Sekta binafsi liliwahusisha sehemu ya watalii 300 waliowasili nchini kwa ziara ya kitalii ya siku nne.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Caesar Waitara kwa pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Jeri Muro wakifuatilia hotuba ya Mhe. Kairuki hayupo pichani
Wadau mbalimbali wakishiriki kongamano hilo
Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki naye akifuatilia matukio wakati wa kongamabo la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na China lililofanyika Arusha
Mhe. Waziri Kairuki akiendelea na hotuba yake huku Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Adolf Mkenda na Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Mhe. Gabriel Daqarro wakisikiliza
Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, Bw. GodfreySimbeye akizungumza
Mdau kutoka China naye akiwasilisha mada
Sehemu ya wawekezaji kutoka China wakifuatilia kongamano lililoandaliwa na Tanzania kwa ajili yao
Sehemu ya wadau kutoka Tanzania nao wakifuatilia kongamano
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mhe. Anthony Mavunde akizungumza na Mhe, Daqarro wakati wa kongamano hilo
Wadau wakifuatilia kongamano
Kongamano likiendelea

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...