Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (AfCHPR) yenye makao yake makuu jijini Arusha itafanya ziara ya kikazi nchini Djibouti ili kukutana na kufanya mazungumzo na wadau mbalimbali kwa lengo la kuiitangaza Mahakama hiyo ya Umoja wa Afrika (AU). 

Ujumbe wa ziara hiyo inayoanza Mei 21 hadi Mei 24 pia unatarajiwa kukutana na Waziri Mkuu wa Djibouti, Waziri wa Mambo ya Nje, Waziri wa Sheria na Spika wa Bunge . 

Rais wa Mahakama ya Afrika, Mheshimiwa Jaji Sylvain Ore’, alisema wakati wa ziara hiyo itaendeshwa semina inayolenga kukuza uelewa wa wadau hao juu ya uwepo wa Mahakama na jinsi inavyoendesha shughuli zake ikiwemo kupokea mashauri. 

Kwa mujibu wa Jaji Ore’,Uelewa wa wadau hao kuhusu uwepo wa AfCHPR pia utaleta hamasa kwa nchi nyingi zaidi za AU kuridhia itifaki iliyoanzisha mahakama hiyo na kutoa tamko rasmi la kutambua na kukubali mamlaka ya Mahakama hiyo kuweza kupokea kesi za watu binafsi na Mashirika yasiyo ya kiserikali(NGOs). 

“Ili Mahakama iweze kufanikisha malengo yake na pia kuimarisha mfumo wa Haki za Binadamu barani Afrika,nchi nyingi za Umoja wa Afrika hazina budi kuridhia itifaki iliyounda Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kwa mujibu wa kifungu cha 34(6)”,Alisisitiza Jaji Ore’. 

Tangu mwaka 2010,Mahakama hiyo ya Afrika imefanikiwa kuendesha programu mbalimbali zinazolenga kutoa elimu ya uwepo wa AfCHPR pamoja na shughuli zake katika baadhi ya nchi za Afrika ikiwemo Chad,Ethiopia,Afrika ya Kusini,Ghana,Malawi,Kenya,Uganda,Zambia,Morroco na Tunisia.Nchi nyingine ni IvoryCoast,Cape Verde,Jamhuri ya Kiarabu ya Sahrawi,Misri na GuineaBissau. 

AfCHPR ilianzishwa mwaka 2006 na ilianza shughuli zake rasmi mwaka 2008.
 African Court in Arusha, Tanzania
Rais wa Mahakama ya Afrika, Mheshimiwa Jaji Sylvain Ore’,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...