Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele amekutana na Wabunge wapya wa Bunge la Afrika wataoapishwa siku ya Jumatatu Mei 6,2019 wakati wa Mkutano wa Pili wa Bunge la Tano la Bunge la Afrika jijini Johannesburg Afrika kusini.
Mkutano huo wa kuwajengea uwezo kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu Bunge la Afrika ikiwemo kuwaeleza historia na jinsi bunge hilo linavyofanya kazi umefanyika katika ukumbi mdogo wa makao makuu ya Bunge la Afrika uliopo Midrand,jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini.
Mheshimiwa Masele ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini nchini Tanzania,amewapongeza hao wabunge 26, kutoka nchi tano zikiwemo Eswatini, Msumbiji, Uganda, Zambia na Algeria kwa kuchaguliwa kuwakilisha katika Bunge la Afrika.
Kikao cha Pili cha kawaida cha Bunge la Tano la Afrika kinatarajiwa kuanza siku ya Jumatatu Mei 6,2019 ambapo wabunge zaidi ya 250 watajadiliana juu ya kauli mbiu ya Umoja wa Afrika ya mwaka huu “Mwaka wa Wakimbizi na Watu Waliopotea” na suluhisho la kudumu juu ya tatizo la wakimbizi barani Afrika.
Mijadala mingine itahusu  taarifa juu ya amani na usalama katika bara ikiwa ni pamoja na maendeleo ya hivi karibuni na hali ya kisiasa Libya, Sudan, Algeria na mchakato wa amani nchini Sudan Kusini. 
Na Kadama Malunde – Johannesburg,Afrika Kusini.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele akizungumza wakati wa mkutano na wabunge wapya wa Bunge la Afrika leo,katika ukumbi mdogo wa Bunge la Afrika,Johannesburg nchini Afrika Kusini 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele akiwakaribisha wabunge wapya wa Bunge la Afrika.
Sehemu ya wabunge hao wakimsikiliza Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele akielezea jinsi Bunge la Afrika linavyofanya kazi.
Sehemu ya wabunge hao wakiwa ukumbini.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele akizungumza ukumbini.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele akiwaelezea jambo wabunge hao wakati akiwatembeza katika jengo la ofisi za utawala za Bunge la Afrika.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele akielezea jambo wakati wabunge wapya wa Bunge la Afrika wakitembelea ofisi za Bunge la Afrika nchini Afrika Kusini.
Mheshimiwa Masele akiwaeleza jambo wabunge hao.
Mheshimiwa Masele akizungumza na wabunge hao.
Mheshimiwa Masele akiwaeleza jambo wabunge hao.
Picha ya pamoja,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele na wabunge wapya wa Bunge la Afrika.
Picha ya pamoja,Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika Mheshimiwa Stephen Masele na wabunge wapya wa Bunge la Afrika. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...