Klabu ya Manchester City imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Soka nchini humo baada ya leo kuifunga klabu ya Brighton goli 4-1 na kufikisha alama 98.
-
Man City inachukua ubingwa huo huku Liverpool iliyokuwa inaipa ushindani mkubwa inamaliza nafasi ya pili baada ya leo kuifunga klabu ya Wolves goli 2-0 na kufikisha alama 97

Man City imetetea kombe hilo baada ya msimu uliopita kuwa mabingwa na hili ni kombe lao la nne ndani ya kipindi cha misimu 8 iliyopita

Nafasi ya 3 imechukuliwa na Chelsea yenye alama 72, nafasi ya 4 imechukuliwa na Tottenham yenye alama 71, Arsenal imechukua nafasi ya 5 baada ya kupata alama 70 huku Manchester United ikiwa nafasi ya 6 na alama 66

Kwa msimamo huo, vilabu vya Manchester City, Liverpool, Chelsea na Tottenham vimekata tiketi ya kushiriki michuano ya Klabu Bingwa Ulaya kwa msimu wa 2019/2020

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...