Maofisa wa Idara ya Ujasusi nchini Kenya wanaelekea Dubai ili kuchukuwa taarifa ya mwakilishi wa Umoja wa Falme za Kiarabu kuhusiana na sakata la dhahabu bandia linalochunguzwa.

Wakati huohuo, pirikapirika zinaripotiwa Bungeni za kusaka saini ili kumtimua Waziri wa Usalama wa Taifa, Fred Matiangi, kwa madai ya kuwalinda watuhumiwa wa kashfa hiyo. 

Jeshi la Polisi la nchini humo linawashikilia maofisa Polisi waliokuwepo kwenye eneo ilikopatikana dhahabu hiyo bandia wakiwa wanawalinda wanadiplomasia na wala sio wahalifu. 

Maofisa wa Idara ya Ujasusi walitazamiwa kusafiri jioni ya leo Jumanne (21 Mei) kuelekea Dubai ili kuchukuwa taarifa ya mwakilishi wa Umoja wa Falme za Kiarabu kuhusu sakata hilo la dhahabu bandia linalochunguzwa. 

Majasusi hao walitazamiwa kumhoji Ali Zandi anayemuwakilisha Sheikh Mohammed Bin Rashid Al Maktoum na kampuni ya Zlivia inayofanya biashara ya dhahabu Dubai.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...