Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera aliyevaa suti akiangalia moja ya mashine ya kufyatulia tofali alipotembelea chuo cha Ufundi kinachomilikiwa na taasisi ya Kiuma,kulia mwalimu wa Useremala wa chuo hicho Patrick Komba,
Mwenyekiti wa Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kiuma Dkt Matomora Matomora kushoto akimueleza jambo jana Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera juu ya vijana wa Tunduru kushindwa kujitokeza kujiunga na chuo cha Ufundi jambo lililochangia vijana wengi wilayani Tunduru kuwa maskini.
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera kushoto akipokea Bendera ya Chama cha Wananchi cuf kutoka kwa aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji cha Fundimbanga kupitia chama hicho ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi,hata hivyo katika mkutano huo Mkuu wa wilaya alilazimika kutimua mbio baada ya kutokea kwa Nyoka watatu kutoka juu ya Mti hivyo kusababisha taharuki kubwa kwa Wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Picha na Muhidin Amri
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...