Na.Vero Ignatus,Arusha.

 Mdahalo wa wanawake vijana umefanyika Jiiini Arusha ukiwa na lengo la kukuza sauti na ushiriki wa wanawake vijana kwenye sera zinazohusu Afya zao.

Odero Charles Odero ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Uraia na msaada kisheria amesema wanafanya kazi na makundi mbalimbali ya wanawake haswa katika maeneo ya Demokrasia,haki za binadamu,utawala bora kwa jamii zile ambazo haziwezi kujiwakilisha kupata haki zao.

Amesema lengo la mradi huo wa miezi 3 ni kukuza sauti za wanawake vijana ambao wapo kwenye rika  balehe katika sera zinazohusu maisha na afya zao,kuwatia vijana hamasa ili waweze kushiriki katika sera zinazohusu maisha yao  kwani asilimia kubwa ya wanawake hawashiriki maamuzi yanayowahusu

Uzoefu wetu kama shirika ndani ya miaka 5 sasa ukienda kwenye mikutano mbalimbali ya vijiji wanawake hawashiriki kutoa maamuzi.

Dkt.Eliamani Laltaika ni mkufunzi kutoka chuo cha Nelson na muwezeshaji wa mdahalo huo, ameainisha kuwa 75% ni Vijana na wanahitaji Sera ya maeneo maalumu  ili waweze kutambuliwa ambapo inakwenda sambamba na Elimu ya Ufundi Sayansi na Teknolojia ili aweze kujitegemea mahusiano,Elimu ya Afya ya uzazi.

Amesema vijana wanatakiwa kupaza sauti kwani wanayo matamanio katika maisha kwasababu vyombo vya maamuzi vinatakiwa vielewe mahitaji ya vijana ili waweze kupata msaada na kutambua nguvu kazi.

Amesema kuwa njia ambazo zinatumika kupaza sauti kijana anatakiwa ajitambue yeye ni nani,ajielewe,ajiheshimu,aseme asikike,ajiunge pamoja ili kubadilishana uzoefu,kwakutumia vyombo vya serikali,Mashirika yasiyo ya kiserikali na mitandao ya kijamii.

Dkt.Laltaika amewataka vijana kutumia mitandao ya kijamii vizuri kwa faida ili  sauti kwani shughuli zote za kijamii ikiwemo Biashara  zinapatikana humo,ila pia lazima watambue zipo changamoto,athari pamoja na faida katika mitandao ya kijamii katika kuleta haki za vijana.

Mwenyekiti wa Maendeleo ya Jamii Jiji la Arusha na Diwani wa Kata ya Ngarenaro Isaya Doita amesema Kumpiga mwanamke ni kosa ,ni udhakikishaji wa kijinsia hivyo amewataka wanawake pale wanapoona vitendo vya udhalikishaji watoe taarifa katika vyombo vya sheria na watapatiwa msaada mara moja.

Mradi huo umewezeshwa na shirika la SAT,eannaso,Hervoice kuweza kupaza sauti Mradi unaitwa kukuza sauti za vijana ambapo ni mradi wa miezi mitatu.zaidi ya vijana wanawake 40 wameshiriki mjadala huo ambao umeshirikisha watunga sera,kamati ya Afya na Elimu
Mkufunzi kutoka chuo cha Nelson Mandela Dkt.Eliamani Laltaika,na muwezeshaji wa  Mdahalo wa siku moja kuhusiana na kukuza sauti kwa wanawake vijana kuhusiana na Sera zinazohusiana na Afya zao
Odero Charles Odero ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Uraia na msaada kisheria (CiLAO)akizungumza na wanawake katika mdahao wa siku moja uoiofanyika Jiiiji Arusha.
Mwenyekiti wa Maendeleo ya Jamii Jiji la Arusha na Diwani wa Kata ya Ngarenaro Isaya Doita :Kumpiga mwanamke ni kosa ,ni udhakikishaji wa kijinsia.
Baadhi ya washiriki wa msahalo wa msahalo wa siku moja wa wananawake vijana ,pia waliweza kuzungumzia matumizi ya mitandao ya kijamii kwa vijana ,athari,changamoto,faida zake katika kupaza sauti za vijana.
Muwezeshaji wa Mdahalo huo Dkt. Eliamani Laltaika,akiwa anampatia kitabu alichokiandika ,Mkurugenzi wa Taasisi ya Uraia na msaada kisheria (CiLAO)Odero Charles Odero.
Washiriki wa mdahalo wakifuatilia mada zilizokuwa zinaendelea ikiwemo ya mikakati ya utekelezaji wa sera za vijana,Ushiriki wa wanawake na uongozi wa serikali za mitaa,vitongoji,vijiji na mitaa.
Mmoja wawaandishi akichangia mada katika msahalo huo wawanawake vijana uliofanyika jijini Arusha.
 Emma Ally Kimambo akijibu swali aliloulizwa na Mkugunzi wa Chuo Kikuu ca Nelson Mandela Dkt .Laltaika.
Baadhi ya Wanawake vijana wakifurahia jambo katika Mdahalo wa kukuza sauti kwa wanawake vijana kuhusiana na Seea zinaazohusiana na Afya zao.
Washiriki pia wakiwa darasani katika msahalo huo wa siku mojankama inavyoonekana pichani.
Mijadala katika makundi yalioundwa katika mdahalo huo.
Mkufunzi kutoka chuo cha Nelson Mandela Dkt.Laltaika akiwaonyesha wanawake vijana namna ya kutumia mtandao wa kijamii wa Twita kama #tag inavyoonekana hapo.
Mazoezi yalikuwa moja ya somo katika mdahalo huo kana inavyoonekana pichani.
Picha ya pamoja baada ya Mdahalo kumalizika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...