Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mhandisi, Dkt. Samuel Gwamaka ametembelea kiwanda kinachojishughulisha na uzalishaji wa mifuko mbadala ili kujionea kiasi cha uzalishaji na uhakika wa upatikanaji wa mifuko hiyo.

Dkt. Gwamaka alifurahia ufanyaji kazi wa kiwanda hicho kinachomilikiwa na watanzania, kwasababu asilimia 90 ya malighafi wanazotumia zinatoka hapahapa Tanzania. Vilevile tayari kimeajiri watu zaidi ya 25, na vibarua zaidi ya 45. Aliongeza kuwa kwasasa Serikali ipo tayari kuwasaidia wale wote ambao wanataka kujikita kwenye uzalishaji wa mifuko mbadala.Alimalizia kwakuwatoa wasiwasi wananchi kuhusu upatikanaji wa mifuko mbadala nakusema kuwa wananchi wafate sharia kwasababu katazo la mifuko ya plastiki ni kwaajili ya kulinda mazingira na afya zao pia.

Kwa upande wa waendeshaji wa kiwanda hicho, wamesema kuwa wamefurahia katazo la mifuko ya plastiki kwani wanaamini kutokana na mahitaji ya mifuko mbadala kuwa mingi watazidi kuongeza ajira kwa kinamama na vijana ukizingatia uzalishaji wa mifuko hiyo hauhitaji elimu kubwa ya darasani.
Dkt. Gwamaka akipatiwa maelezo na wahusiki wa kiwanda cha mifuko mbadala namna ambavyo wanaweza kutengeneza mifuko mbadala ambayo itakuwa na uwezo wa kubeba vitu vyenye asili ya maji maji. 
Dkt. Gwamaka akipewa maelezo na namna ambayo mashine zinavyofanya kazi. 
Dkt. Gwamaka akipewa maelezo na namna ambayo mashine zinavyofanya kazi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...