Naibu waziri wa Madini Stanslaus Nyongo akionyesha jiwe la madini ya Almasi lenye uzito wa “ct” 512.15 leneye thamani Tsh. Bilion 3, 262, 149, 332.75 mali ya mchimbaji mdogo bwana Joseph mkazi wa Shinyanga. Kushoto kwake ni Kamishna wa Madini Prof. Mruma na kulia kwake ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko. 
Kamishna wa Tume ya Madini Prof. Mruma akimuonyesha jambo Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo jiwe la madini ya Almasi lenye uzito wa “ct” 512.15 leneye thamani Tsh. Bilion 3, 262, 149, 332.75 wakati wa mauzo yake yaliyofanyika katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga. 
Bi. Dorcas Moshi, Mchambuzi na Mthamini wa Madini ya Vito na Almasi kutoka tume ya Madini akiifunga rasmi Almasi ya Josephy Temela mara baada ya kukamilika kwa taratibu za uthaminishaji na kupata ghara halisi huku ikishuhudiwa na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo mwenye suti ya Blue. 
Bw. Joseph Temba mchimbaji mdogo ambae ameuza jiwe lake la madini ya Almasi lenye uzito wa “ct” 512.15 leneye thamani ya Tsh. Bilion 3, 262, 149, 332.75 wakati wa mauzo yake yaliyofanyika katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga. 


Na: Issa Mtuwa (Wizara ya Madini) – Shinyanga 

Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, ameshuhudia mchimbaji
mdogo wa madini ya almasi bwana Joseph akijizolea fedha, dola za
kimarekani (USD) milioni 1, 418,510.82 ambazo sawa na Tsh. bilioni 3,
262,149,332.75 kutokana na mauzo ya jiwe moja lenye uzito wa Kareti
(ct)512.15. Shuguli ya mauzo ya Almas hiyo imefanyika leo tarehe
25/05/2019 katika soko la Madini la mkoa wa Shinyanga na kushuhudiwa
pia na Kamishna wa Tume ya Madini Prof. Mruma na vyombo mbalimbali
vya usalama na wawakilishi wa benki ya CRDB Shinyangai. 

Akiongea wakati wa kushuhudia mauzo hayo , Naibu waziri Nyongo
amesema, kutokana na mauzo hayo serikali itapata USD 103,551.29 sawa
na Tsh. milioni 238,136,901.61. Ameongeza na kusisitiza kuwa, adhima ya
serikali ya awamu ya tano ni kuwezesha shuguli za wachimbaji wadogo na
wadau wote wa sekta ya madini kufanyika kwa utaratibu unao eleweka
kwa faida yao na ya serikali. 

“Nimpongeze bwana Joseph ambae anauza almasi yake hapa leo kwenye
soko hili la madini, kila kitu kinakuwa wazi mbele ya serikali, polisi, watu wa
usalama na wawakilishi wa Bank ya CRDB, bila usumbufu wowote, na hiki
ndicho tunachokitaka sisi kama serikali, wachimbaji wote kufuata utaratibu
tuliouweka.

Niwaombe wachimbaji kwa mara nyingine, acheni kuuza madini
mchochoroni haita wasaidia zaidi ni kuhatarisha usalama wenu, na pengine
hata kupunjwa kutokana na kuto kujua thamani halisi na bei ya madini yenu
igeni mfano wa bwana Joseph, na niwaambie ukweli ukikamatwa unauza
madini nje ya soko madini hayo yanataifishwa, hivyo utakuwa umekula
hasara na utachukuliwa hatua za kisheria.” amesema Nyongo. 

Kwa upande wake Afisa msaminishaji madini kutoka tume ya Madini Bi.
Dorcas Moshi, Mchambuzi na Mthamini wa Madini ya Vito na Almasi
kutoka tume ya Madini aliekuwa anafanya shuguli nzima ya uthaminishaji
wa Almasi hiyo, amefafanua kuwa fedha iliyopata serikali, Milioni
238,136,901.61 inajumuisha Mrabaha wa USD 85,110.65 sawa na Tsh.
Milioni 195,728,959.97, Ada ya ukaguzi ni USD 14,185.11 sawa na Tshs.
32, 621, 493, .33 na Mrabaha wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu ilikotokea Almasi hiyo (Service Levy) ni USD 4,255.53 sawa na Tsh. 9,
786,448. 

Kwa upande wake Kamishina wa Madini prof. Mruma amewasisitiza
wachimbaji wadogo kuzingatia sheria na taratibu hususani kuchimba
kihalali kwa kuhakikisha wanakuwa na leseni za uchimbaji na kulipa tozo
zote za serikali kwani serikali ipo kwa ajili yao hivyo hawana sababu ya
kuikwepa. 

Kwa upande wake bwana Joseph mmiliki wa almasi hiyo, ameishukuru
Wizara ya madini na Tume ya madini kwa utaratibu waliouweka katika
kutoa muongozo na usimamizi wa namna ya mauzo ya madini
unavyotakiwa kufanyika, ulinzi wa madini yao pindi wanapoyapata na
ametoa wito kwa wachimbaji wadogo wenzake kuwa hakuna sababu ya
kuyakimbia masoko yaliyoanzishwa na serikali kwani yanafaida nyingi
ikiwemo usalama, ulinzi, uwazi na utambuzi wa thamani halisi ya madini
kitu ambacho nadra sana kwenye masoko yasiyo rasmi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...