Na Ripota Wetu
WIZARA ya Ulinzi ya Marekani imesema kwa sasa inapitia ombi la jeshi la nchi hiyo la kutaka kupeleka wanajeshi zaidi ya 5,000 Mashariki ya Kati, wakati wasiwasi ukiongezeka kati yake na Iran.
Taarifa inaeleza kuwa kulingana na maofisa wawili waliozungumza na Shirika la Habari la Reuters kwa masharti ya kutotajwa majina, ombi hilo limewasilishwa na makao makuu ya jeshi la Marekani, lakini bado haiko wazi iwapo wizara hiyo italiidhinisha.
Mmoja wa maofisa hao amesema wanajeshi hao wanapelekwa kwa ajili ya kujihami na hilo linatajwa kama ombi la karibuni zaidi la kuongezwa kwa wanajeshi katika kile ambacho Marekani inakitaja kama kitisho dhahiri kutoka kwa Iran dhidi Marekani na maslahi yake katika ukanda wa Mashariki ya Kati.
Hata hivyo, wizara hiyo ilipoulizwa iwapo kuna ombi hilo ilikataa kuzungumzia mipango yake ya usoni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...