Program Coordinator wa Agitos Foundation Bi Sheila Cleo Mogalo ambaye aliwasili  nchini siku ya Jumanne 7 may 2019 jumamosi May 11, 2019 ametembelea mazoezi ya KUOGELEA ya  watu wenye ulemavu. Mazoezi ya watu wenye  ulemavu yamefanyika katika  bwawa la kuogelea la shule ya Nordic iliyoko Masaki, Dar es salaam. Bi Sheila alifuatana na Katibu Mkuu wa Tanzania Paralympic Committee (TPC) Bwana Tuma Dandi katika kuangalia maendeleo ya michezo ya watu wenye ulemavu.
Bi Sheila aliweza kuzungumza na Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu ndugu Ramadhana Namkoveka jinsi anavyoendesha mafunzo yake, anavyopata waogeleaji, kuwaandaa na changamoto mbalimbali anazokutana nazo . 
Ramadhan Namkoveka alimuarifu kuwa anapata waogeleaji kutoka katika taasisi mbalimbali kama Watoto Kwanza ya Kawe, shule za msingi na wengine ambao wanatoka katika mitaa. Mafunzo hayo ambayo anayatoa bila gharama yoyote, alisema changamoto kubwa ni kupata bwawa la kuogelea ambalo atapata nafasi ya kufanyia mafunzo. 
Aidha Namkoveka ameshukuru uongozi wa shule ya Nordic iliyoko Masaki Dar Es Salaam kuweza kuruhusu bwawa lake kutumika na kuipa nafasi mchezo wa kuogelea hasa kwa watu wenye ulemavu. 
Hakika imeweza kuzalisha waogeleaji wapatao 14 wenye ulemavu mpaka hivi sasa ambapo mmojawao Gerald Hamisi Sokolo ameweza kushiriki mashindano ya kimataifa kwa kushiriki mashindano yaliyofanyika Nairobi Kenya tarehe 8-11 Februari 2018. 
Gerald ni mtanzania pekee kwa upande wa kuogelea kuweza kutambuliwa na Chama cha Kuogelea cha dunia (World Para Swimming).Pia hivi sasa juhudi juhudi zinafanyika kuweza kuwapeleka wachezaji katika mashindano ya kimataifa kabla ya mashindano ya Paralympic yatakayofanyika Japan 2020.
Sheila amependa hali ya michezo kwa watu wenye ulemavu ilivyo hapa nchini na akasema kuwa juhudi kubwa zinatakiwa zifanyike katika awareness ili walemavu wengi waweze kushiriki katika michezo yote. Sheila ameondoka siku ya Jumatatu  tarehe 13 May 2019 na kurudi Bonn Ujerumani ambako ndiko kwenye makao makuu ya Agitos Foundation ambao ni washirika wakubwa wa International Paralympic Committee (IPC)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...