* Akumbusha waajiri kuwaajiri walemavu kama sheria inavyosema
*Awapongeza wafanyakazi kwa juhudi wanazozifanya katika ujenzi wa taifa
Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amemuagiza Katibu tawala wa Mkoa na Wakurugenzi wa Halmashauri zote jijini humo kuhakikisha wanawapandisha madaraja Watumishi wanaostahili ndani ya mwezi mmoja kuanzia leo.
Makonda ametoa agizo hilo wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi duniani (Mei Mosi) ambayo Mkoani humo yameadhimishwa katika uwanja wa uhuru jijini humo, amesema kinachomshangaza ni kuona wafanyakazi wanaostahili kupandishwa madaraja hawapandishwi licha ya kuwa na sifa na vigezo vinavyostahili.
Aidha Makonda amewaagiza maafisa kazi kushughulikia kero za wafanyakazi kwa wakati ili watumishi wafanye kazi zao bila vikwazo.
Pamoja na hayo Makonda amewataka waajiri kuhakikisha watumishi wanafanya kazi katika mazingira bora na salama huku akiwakumbusha kuajiri walemavu kama sheria inavyowataka.
Hata hivyo amehimiza watumishi kujituma katika kazi wanazofanya huku akiwapongeza walimu na watumishi wengine kwa juhudi za kushughulikia kero za wananchi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda akizungumza na wafanyakazi pamoja na wakazi wa Dar es salaam wakati wa maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi duniani Mei Mosi yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...