JOSEPH MPANGALA 

Serikali iko Mbioni Kujenga Kiwanda cha Mvinyo pamoja na Juise kutokana na Mabibo ya korosho ambayo yamekuwa yakitupwa mara baada ya korosho kuuzwa na hivyo Wakulima kukosa fedha za ziada kutokana na Tunda hilo.

Akiuliza swali la Nyongeza Katika Mkutano wa 15 kikao cha 29 Mbunge wa Ndanda Cecil Mwambe amehoji Utafiti uliokuwa ukifanywa na Chuo cha Naliendele kilichopo Mtwara kuhusu Kochoko au mabibo ya Korosho umefikia wapi Mpaka sasa kwa lengo la Kuwawezesha wakulima Kuweza kujinufaisha zaidi na zao la korosho.

“Kochoko ni zile washi zinazotokana baada ya mavuno ya korosho wakulima huwa wanazitupa na wengine huwa wanaziuza na wengine wanatengeneza Gongo na inafahamika kwamba Gongo sio pombe haramu isipokuwa namna inavyotengenezwa je Utafiti uliokuwa Ukifanywa na Chuo cha naliendele Umefikia wapi”?

Akijibu swali hilo Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga amesema kupitia Chuo cha Utafiti cha Naliendele tayari wamefanya Utafiti na kutoa maagizo ya ujengwaji wa kinu ili kuweza kuzalisha Mvinyo pamoja na juisi itakayotokana na mabibo kwa lengo la kuongeza thamani zao la Korosho.              

“Ni kweli kabisa chuo chetu kupitia tawi letu la Naliendele tumefanya utafiti wa kina na tumebaini kwamba kuna mazao mengi tunaoweza kuzalisha kutokana na Korosho ikiwemo Juisi na ikiwemo mvinyo maalum unaotokana na mabibo ya Korosho na tumetoa maagizo kwenye tawi letu sasa hivi kujenga kinu cha kuweza kuchakata ili tuweze kuzalisha mvinyo pamoja na juisi ambayo tutaiuza hapa Nchini na hivyo itaongeza thamani na mapato yatakayotokana na zao la Korosho” amesema Hasunga Waziri wa Kilimo.
Mbunge wa Ndanda Cecil Mwambe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...