Msafara wa wachezaji 18 na viongozi wa Klabu ya Sevilla FC umetua nchini usiku wa kumkia leo . 

Sevilla wametua nchini chini ya uratibu wa Kampuni ya Kubashiri Matokeo ya SportPesa pamoja na Laliga. Sevilla wakiwa hapa nchini watacheza mchezo mmoja wa kirafiki dhidi ya Simba kesho kutwa Alhamisi utakaopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya Sevilla kutua, Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa, Tarimba Abbas amesema kuwa anafurahia ujio wa Sevilla ambao utaongeza utalii nchini.

Tarimba aliwatahadharisha Sevilla kwa kuwaambia kuwa wajiandae wanacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Mabingwa wa Ligi Kuu Bara.
“Ninawaambia kuwa jiandaeni kupambana na mabingwa wa ligi hapa nchini ambao ni Simba.” Ni timu nzuri iliyojiandaa kuhakikisha inapata ushindi kutokana na ubingwa walioupata,”amesema Tarimba.

Lakini pia mara baada ya kuwasili nchini,kikosi hicho kililakiwa na burudani sana kabisa kabisa kutoka kwa kundi la Ngoma za asili linaloongozwa na Msanii mahiri wa kughani Mrisho Mpoto,ama kwa hakina walikunwa na uchezaji ngoma na kujikuta nao wakiinuka kujimwaya mwaya kwa pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...