Afisa Elimu kwa Walipakodi TRA Kanda ya Kaskazini Eugenia Mkumbo amesema kuwa Mamlaka hiyo inatoa fursa kwa wafanyabiashara wanaolalamikia kukadiriwa kodi ya juu kuliko kipato chao.
Mkui wa Wilaya ya Arusha Gabriakizindua wiki ya mlipa kodi iliyofanyika eneo la stendi kuu ya Mabasi ya mikoani,ambapo ameitaka TRA 
Baadhi ya wananchi waliojitokezankatika uzinduzi wa wiki ya Elimu kwa mpiga kodi iliyoansaliwa na Mamlaka ya Matapo nchini TRA Jijini Arusha



Na Vero Ignatus ,Arusha.

Mamlaka ya Mapato TRA mkoa wa Arusha imetakiwa kuimarisha ukaguzi wa mashine za kielektroniki ili kuwabaini wafanyabiashara wanaokwepa kodi na kuikosesha serikali mapato ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua Kali za kisheria. 

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro amesema hayo wakati akizindua wiki ya mlipa kodi iliyofanyika eneo la stendi kuu ya Mabasi ya mikoani,ambapo ameitaka TRA kuhakikisha kuwa wanakagua na kuwabaini wafanyabiashara wasiotoa risiti na kuikosesha serikali mapato jambo ambalo ni uhujumu uchumi.

Aidha amewataka Wafanyabiashara kutoa taarifa za siri juu ya baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu wanaokwepa kodi ili hatua Kali zichukuliwe juu yao.
Kaimu Meneja wa TRA mkoa wa Arusha Irine Donald amesema kuwa wataendelea kushirikiana n wafanyabiashara katika kutatua changamoto na kero zao ili waweze kufurahia kulipa kodi ya serikali.

Kwa upande wao wafanyabiashara Elisante Mungure na Winifrida Massawe Wafanyabiashara. wamelalamikia uwepo wa wamachinga mbele ya maduka yao huku wakiuza bidhaa zinazofanana hivyo kukosa soko la bidhaa zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...