Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe akiongoza kikao kazi cha majumuisho ya ujumbe kutoka Benki ya Dunia kuhusu ufuatiliji wa utekelezaji wa Mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga (Expanding Rice Production project), Kilichofanyika Jijini Dar es salaam tarehe 22 Mei 2019.
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe akiongoza kikao kazi cha majumuisho ya ujumbe kutoka Benki ya Dunia kuhusu ufuatiliji wa utekelezaji wa Mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga (Expanding Rice Production project), Kilichofanyika Jijini Dar es salaam tarehe 22 Mei 2019.



Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam

Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe ameengoza kikao kazi cha majumuisho ya ujumbe kutoka Benki ya Dunia kuhusu ufuatiliji wa utekelezaji wa Mradi wa kuongeza tija na uzalishaji wa zao la mpunga (Expanding Rice Production project), mradi ambao unatekelezwa Tanzania bara na Zanzibar. 

Kikao hicho cha majumuisho kimefanyika leo leo Tarehe 22 Mei 2019 katika ukumbi wa ofisi ndogo za Wizara ya Kilimo maarufu kama Kilimo 1 Jijini Dar es salaam.

Ujumbe huo kutoka Benki ya Dunia ukiongozwa na Bi Sarah Simons umeeleza kuridhishwa na kasi ya utendaji kazi katika utekelezaji wa kazi za mradi huo kulingana na malengo yaliyowekwa kwa kipindi cha miezi 6 iliyopita. 

Ujumbe huo ulianza kazi ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mradi huo wa ERPP tarehe 19-21 Mei 2019 ambapo walitembelea Tanzania bara na Zanzibar na walikutana katika wizara ya Kilimo (Bara) na Wizara ya kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi (Zanzibar) na wameshukuru ushirikiano walioupata kwa watendaji wanaosimamia mradi huo.

Aidha ujumbe huo pamoja na kusisitiza kasi ya utekelezaji na ukamilishaji wa kazi za Mradi huo pia waliridhishwa na namna ambavyo mradi umekuwa ukiripoti kuongezeka kwa uzalishaji wa mpunga kwa hatua za awali baada ya wakulima kutumia mbegu bora katika mfumo wa kilimo shadidi (SRI). 

Pia maendeleo mazuri katika maandalizi ya ujenzi wa miundombinu ya Umwagiliaji na Maghala kwa kipindi cha miezi sita iliyopita na wamekuwa na matumaini kuwa Ujenzi wa miradi hiyo na kazi zingine zitakamilika kabla ya tarehe ya mwisho ya mradi huo. 

Mhandisi Mtigumwe (Katibu Mkuu Kilimo Tanzania bara) ameushukuru ujumbe huo na kuwaeleza kuwa wataendelea kwa kasi kutekeleza shughuli zilizobaki za mradi huo ili tija kwa wakulima na nchi ionekane. 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Maliasili, Mifugo na Uvuvi Bi Mansura Kassim aliushukuru Ujumbe huo kwa ufuatiliaji wao na kueleza kuwa Kwa upande wao wataendelea kukamilisha kazi zilizobakia katika mradi na kusimamia mradi huo ipasavyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...