Waziri wa Kilimo, Mhe Japheth Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akifungua Jukwaa la Fikra la Mwananchi, lililofanyika katika ukumbi wa Milleinum Tower Jijini Dar es Salaam, tarehe 23 Mei 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Waziri wa Kilimo, Mhe Japheth Hasunga (Wa nne kulia) akifatilia mada mbalimbali mara baada ya kufungua Jukwaa la Fikra la Mwananchi, lililofanyika katika ukumbi wa Milleinum Tower Jijini Dar es Salaam, tarehe 23 Mei 2019.
Waziri wa Kilimo, Mhe Japheth Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akifungua Jukwaa la Fikra la Mwananchi, lililofanyika katika ukumbi wa Milleinum Tower Jijini Dar es Salaam, tarehe 23 Mei 2019.
Waziri wa Kilimo, Mhe Japheth Hasunga (Wa nne kulia) akifatilia mada mbalimbali mara baada ya kufungua Jukwaa la Fikra la Mwananchi, lililofanyika katika ukumbi wa Milleinum Tower Jijini Dar es Salaam, tarehe 23 Mei 2019.



Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam

Kumekuwa na mwamko mkubwa na muitikio mahusiusi wa vijana kuingia katika shughuli za kilimo tofauti za siku za nyuma ambapo ilikuwa ni vigumu kukuta vijana wakishawishika kuingia katika kilimo. 

Takwimu za mwaka 2014 za Integrated Labour Force Survey chini zinaonesha kwamba vijana ni asilimia 56 ya nguvu kazi ya Taifa. Hivyo, wakihusishwa na kuwezeshwa ipasavyo kwa kuwavutia kwa kuzingatia mahitaji yao ya msingi katika kuwekeza katika kilimo, vijana hawa watalifikisha Taifa katika maendeleo chanya.

Waziri wa Kilimo, Mhe Japheth N. Hasunga (Mb) ameyasema hayo Leo Tarehe 23 Mei 2019 wakati akifungua Jukwaa la Fikra la Mwananchi, lililofanyika katika ukumbi wa Milleinum Tower Jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa Wizara ya Kilimo ina Mkakati wa Taifa wa Vijana wa kuwawezesha kushiriki katika kilimo kwa kuzingatia malengo makuu kumi (10) yakiwemo upatikani wa ardhi, upatikanaji wa mitaji, mafunzo ya ujasiriamali na uhakika wa masoko ya bidhaa zao. 

“Swali kubwa na msingi hapa ni je, sisi wadau wote kwa ujumla tunayatekeleza haya ili kuwavutia vijana kuweza kushiriki uwekezaji katika kilimo kupitia mnyororo wa thamani? Kwani tunakwama wapi?” Aliuliza Mhe Hasunga

Alisema kuwa ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya 2025 ya kufikia uchumi wa kati wa viwanda kunahitajika kilimo bora kitakachowezesha upatikanaji wa malighafi za kutosha kutumika katika viwanda. 

Vilevile, Kilimo chenye tija pia kitawezesha kipato cha wakulima kuongezeka na hivyo kuwezesha wananchi wengi kufikia kipato cha kati. “Nina uhakika ifikapo mwaka 2025 tunaweza kufikia uchumi wa kati na pengine na kuzidi kiwango hicho tulichojiwekea na hapo tutaiona Tanzania mpya yenye neema” Alisema

Mhe Hasunga alieleza kuwa Wizara ya Kilimo imeanza kufanya marekebisho ya Sera ya Kilimo na kutunga Sheria ya Kilimo, hatua ambazo zitaimarisha usimamizi na kutoa mwongozo wa maendeleo ya sekta ya kilimo kwa ujumla.

Kongamano hilo pla Jukwaa la Fikra au Mwananchi Thought Leadership Forum (MTLF) lilirushwa mubashara na Kituo cha Matangazo cha ITV pamoja na Radio One Sterio likiwa na lengo la kujadili masuala yanayowagusa Watanzania moja kwa moja kwa lengo la kuyatafutia suluhisho kwa pamoja kupitia mijadala iliyotolewa.

Alisema tangu majukwaa ya namna hiyo yalipoanza mwaka 2018 yakihusisha pia IPP Media (ITV, Radio na Capital Radio) masuala kadhaa yamejadiliwa ikiwa pamoja na mada za kuvutia kama vile "Magonjwa Yasiyoambukiza", mada ya "Tanzania ya Viwanda" na masuala ya Mazingira. Kupitia jukwa hili, Mamilioni ya Watanzania wamefaidika kwa kutoa na kusikiliza maoni katika Nyanja hizo kupitia mitandao ya jamii, televisheni, radio na magazeti. 

Mhe Hasunga alisisitiza kuwa Serikali haiwezi kufikia malengo yake bila kuwashirikisha wadau, aliwakaribisha wananchi na wadau wote kujadili na kutoa mawazo yatakayo iwezesha wizara ya kilimo kutoka katika hali iliyopo na kwenda hali nyingine ya kuboresha kilimo katika nyanja za masoko, upatikanaji wa pembejeo, wataalamu na zana bora za kilimo. 

Waziri Hasunga aliongeza kuwa Pamoja na umuhimu wa sekta ya kilimo katika kuchangia uchumi kwa asilimia kubwa zaidi kuliko sekta zingine, kuajiri watu wengi zaidi kuliko sekta nyingine, kuwezesha upatikanaji wa chakula cha kutosha hapa nchini na ziada kuuza nje ya nchi, kuchangia fedha nyingi za kigeni na kuwa moja ya sekta mama katika pato la Taifa na nguzo kuu ya uchumi, bado kilimo hakijaweza kukuza uchumi wetu kwa namna inavyostahili kutokana na umuhimu wake. 

“Tunatambua kihistoria kuwa nchi nyingi duniani zilianzia maendeleo kwenye mapinduzi ya kilimo, kwenda mapinduzi ya viwanda, huduma na baadaye teknolojia. Pengine hatuwezi kukwepa kufanya mapinduzi hayo ya kilimo hapa nchini. Tutakachoweza kufanya ni mapinduzi ya kasi zaidi kwa sababu tuna mifano mingi ya kuiga hapa duniani” Alikariiriwa Mhe Hasunga

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...