MSHAMBULIAJI nyota katika Ligi ya Ubelgiji anayekipiga Klabu ya Genk na nahodha wa timu
ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mbwana Samatta huenda akatua Ligi Kuu ya England (EPL) msimu
ujao.
Samatta anayejulikana zaidi kwa jina Samagoal, amedokeza hadi sasa kuna vilabu sita vya Ligi
ya Primia ambavyo vinapigana vikumbo kumsajili nyota huyo ambapo mwenyewe amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akieleza kuwa hayupo katika wakati mzuri kusema klabu gani anaweza kwenda.
Mchezaji huyo amefafanua kutoka Hispania kuna timu mbili ambazo zimekuwa zikiisaka saini
yake lakini ndoto yake kubwa ni kucheza katika Ligi Kuu ya England. Hata hivyo
inaelezwa si mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kudaiwa kuwindwa na vilabu vya Ligi ya
Premia.
CHANZO -BBC
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...