MSHAMBULIAJI nyota katika Ligi ya Ubelgiji anayekipiga Klabu ya Genk na nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mbwana Samatta huenda akatua Ligi Kuu ya England (EPL) msimu ujao.

Samatta anayejulikana zaidi kwa jina Samagoal, amedokeza hadi sasa kuna vilabu sita vya Ligi ya Primia ambavyo vinapigana vikumbo kumsajili nyota huyo ambapo mwenyewe amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akieleza kuwa hayupo katika wakati mzuri kusema klabu gani anaweza kwenda.

Mchezaji huyo amefafanua kutoka Hispania kuna timu mbili ambazo zimekuwa zikiisaka saini yake lakini ndoto yake kubwa ni kucheza katika Ligi Kuu ya England. Hata hivyo inaelezwa si mara ya kwanza kwa mchezaji huyo kudaiwa kuwindwa na vilabu vya Ligi ya Premia. CHANZO -BBC

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...