Irene Donald Meneja msaidizi wa mkoa wa kikodi wa Arusha,Upande wa ukusanyaji wa madeni na ridhaa ya ulipaji kodi.
Mkuu wa wiaya Arumeru Jerry Muro akizungumza katika wiki ya Elimu ya mlipa kodi iliyoandaliwa na TRA Mkoni Arusha.


Na Vero Ignatus,Arusha.

Onyo kali limetolewa kwa Vishoka wanaowatapeli wafanyabiashara kupitia mgongo wa Mamlaka ya Mapato TRA mkoani Arusha waache kufanya hivyo mara moja kwani Mamlaka hiyo itawatachukulia hatua kali za kisheria kwani wanakwamisha ulipaji kodi kwa hiari.

Irene Donald ni Kaimu Meneja wa TRA amesema hayo katika soko la Tengeru alipo alizungumza na walipa kodi katika wiki ya mlipa kodi ,ambapo amesema kuwa kuna baadhi ya watu wanaofahamika kama vishoka ambao hufika TRA na kufanya udanganyifu kwa wafanyabiashara kwa lengo la kujipatia faida huku wakiwaumiza wafanyabiashara.

Jerry Muro ni Mkuu wa Wilaya ya Meru amesema kuwa wafanyabiashara wanapaswa kulipa kodi kwa hiari ili kuchangaia maendeleo ya nchi na kuiwezesha serikali kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi wake.

Baadhi ya wafanyabiashara waliofika kupata elimu ya mlipa kodi Magreth Pallangyo amelalamikia uchafu wa soko la tengeru licha ya kulipa ushuru kwa Halmashauri hiyo hivyo wameiomba serikali itatue changamoto hiyo ili waweze kulipa kodi stahiki.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...