Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo akifungua Mkutano wa Wadau wa NHIF, Mkoa wa Arusha.
Na Mwandishi Wetu, Arusha
SERIKALI imewataka Watoa Huduma waliosajiliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kuachana
na udanganyifu katika utoaji wa huduma kwa wanachama wake kwa kuwa jambo hilo ni kurudisha
nyuma maendeleo ya Mfuko ambao ni nguzo kubwa katika utoaji wa huduma za matibabu.
Akifungua kikao cha Wadau wa NHIF, Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo amesema kuwa udanganyifu
katika huduma ni adui mkubwa wa uimarishaji wa chombo hicho ambacho kwa sasa kinahudumia
wananchi wengi na wanaohitaji huduma ambazo gharama zake ni kubwa.
“Niwaombe sana wadau wote hususan wanachama wa Mfuko, ni vyema kila mmoja kwenye nafasi yake
akawa mlinzi wa huduma anazopata ili Mfuko huu uwe imara zaidi na uendelee kuhudumia wananchi,
mimi binafsi nikiri tu kwamba bila ya kuwa na kadi ya NHIF nisingeweza kumudu gharama za matibabu,
nimemuuguza Mama yangu na alihitaji matibabu yenye gharama kubwa lakini kwa kuwa na kadi ya NHIF
ilinisaidia kwa kiasi kikubwa sana, hivyo ili Mfuko huu uendelee kuwepo ni lazima sote kwa pamoja
tuulinde,” alisema Bw. Gambo.
Kwa upande wa watoa huduma aliwataka kuwa wakweli na kuwa wazalendo katika vipimo na dawa
wanazowaandikia wanachama ili Mfuko uweze kulipa gharama halisi na sio kulipa fedha ambazo
huduma zake hazikuwa sahihi.
“Lengo la Serikali inayoongozwa na Rais wetu Dkt. John Pombe Magufuli ni kuona kila wilaya nchini
inakuwa na Hospitali na kata inakuwa na kituo cha Afya na Kijiji kinakuwa na Zahanati ili upatikanaji wa
huduma za matibabu uwe rahisi na bora zaidi na kwa kutumia mfumo wa Bima ya Afya wananchi
watakuwa na uhakika wa kupata huduma za matibabu wakati wote,” alisema Bw. Gambo.
Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF, Bi. Anne Makinda amesema kuwa Mfuko umejipanga
kuhakikisha mpaka ifikapo mwakani zaidi ya asilimia 50 ya Watanzania iwe inahudumiwa na Mfuko na
kwa upande wa huduma, Mfuko umejipanga kuhakikisha wanachama wake wanapata huduma katika
maeneo yao na kwa ubora unaotakiwa.
Awali akizungumza kwenye mkutano huo Mkurugenzi wa NHIF, Bw.Bernad Konga amebainisha kuwepo
kwa mifumo mizuri ya udhibiti wa udanganyifu ambayo mpaka sasa imeleta matokeo makubwa kwa
kuokoa zaidi ya shilingi Bilioni 4 ambazo zingeweza kulipwa kutokana na vitendo vya udanganyifu vya
baadhi ya watoa huduma.
Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF, Mama Anne Makinda akitoa salaam za Bodi kwa wadau wa Mfuko
huo.
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Bw. Bernard Konga akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji ya Mfuko kwa
wadau wake.
Meneja wa NHIF Mkoa wa Arusha Bw. Isaya Shekifu akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya Mkoa.
Wadau wa NHIF wakifuatilia taarifa mbalimbali za Mfuko.
Sehemu ya Wadau wa Mfuko wakiwa kwenye mkutano huo.
Sehemu ya Wadau wakifuatilia uwasilishwaji wa Mada.
Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu Dkt. David Mwanesano (kulia) akiwa na Meneja Uhusiano wa Mfuko Bi. Anjela Mziray.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...