Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh (wapili kulia) katika kikao cha kujadili uzalishaji wa kasi wa vitambulisho vya taifa nchini, kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma, leo. Pia, viongozi hao walikubaliana kuboresha mitambo ya uzalishaji wa vitambulisho hivyo kwa wingi zaidi. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anord Kihaule. Kulia Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Shaiful Subhan.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh, mara baada ya kumaliza Kikao chao kilichoshirikisha Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na viongozi mbalimbali wa Kampuni hiyo, katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akimsikiliza Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh (wapili kulia), alipokua anafafanua jambo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa wizara hiyo, jijini Dodoma leo. Viongozi wa kampuni hiyo wamekubaliana na viongozi wa Wizara, kufanya kazi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika kuongeza kasi ya uzalishaji wa vitambulisho hivyo. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anord Kihaule. Kulia Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Shaiful Subhan.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akimfafanulia jambo Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh (katikati) katika kikao cha kujadili uzalishaji wa kasi wa vitambulisho vya taifa nchini. Pia, viongozi hao walikubaliana kuboresha mitambo ya uzalishaji wa vitambulisho hivyo kwa wingi zaidi. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo, Shaiful Subhan.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (watatu kushoto), Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu (katikati), Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anord Kihaule (kushoto), pamoja na viongozi mbalimbali wa NIDA, wakiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh (wapili kushoto), na viongozi mbalimbali wa Kampuni hiyo, nje ya jengo la Wizara hiyo, baada ya kumaliza kikao cha kujadili uzalishaji wa vitambulisho vya taifa, jijini Dodoma, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...