Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akizungumza na Rais wa
Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh (wapili
kulia) katika kikao cha kujadili uzalishaji wa kasi wa vitambulisho vya taifa
nchini, kilichofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo, jijini
Dodoma, leo. Pia, viongozi hao walikubaliana kuboresha mitambo ya uzalishaji
wa vitambulisho hivyo kwa wingi zaidi. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anord Kihaule. Kulia Mtendaji
Mkuu wa Kampuni hiyo, Shaiful Subhan.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (kulia) akipokea zawadi
kutoka kwa Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia,
Dato’ Paul Poh, mara baada ya kumaliza Kikao chao kilichoshirikisha
Menejimenti ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa na viongozi mbalimbali wa
Kampuni hiyo, katika kikao kilichofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara
hiyo, jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (katikati) akimsikiliza Rais wa
Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh (wapili
kulia), alipokua anafafanua jambo katika kikao kilichofanyika katika ukumbi wa
wizara hiyo, jijini Dodoma leo. Viongozi wa kampuni hiyo wamekubaliana na
viongozi wa Wizara, kufanya kazi kwa kushirikiana na Mamlaka ya
Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika kuongeza kasi ya uzalishaji wa
vitambulisho hivyo. Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja
Jenerali Jacob Kingu. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya
Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anord Kihaule. Kulia Mtendaji Mkuu wa
Kampuni hiyo, Shaiful Subhan.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola akimfafanulia jambo Rais wa
Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul Poh
(katikati) katika kikao cha kujadili uzalishaji wa kasi wa vitambulisho vya taifa
nchini. Pia, viongozi hao walikubaliana kuboresha mitambo ya uzalishaji wa
vitambulisho hivyo kwa wingi zaidi. Kulia ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni hiyo,
Shaiful Subhan.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola (watatu kushoto), Katibu
Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Jacob Kingu (katikati), Mkurugenzi Mkuu
wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dkt. Anord Kihaule (kushoto),
pamoja na viongozi mbalimbali wa NIDA, wakiwa katika picha ya pamoja na
Rais wa Kampuni ya Iris Corporation Berhard ya nchini Malaysia, Dato’ Paul
Poh (wapili kushoto), na viongozi mbalimbali wa Kampuni hiyo, nje ya jengo la
Wizara hiyo, baada ya kumaliza kikao cha kujadili uzalishaji wa vitambulisho
vya taifa, jijini Dodoma, leo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...