WAZIRI wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora, George Mkuchika amewataka waajili kuwapa ruhusa makatibu mahsusi kuhudhuria semina na vikao, kwani kutokufanya hivyo wanarudisha nyuma maendeleo ya nchi.

Mkuchika ameyasema hayo leo wakati akifungua mkutano mkuu wa saba wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) unaofanyika jijini Arusha na kuwaambia kuwa wao kama Serikali wanaadaa waraka kwa waajili hao kuona umuhimu wa kuwapa ruhusa makatibu hao mahtasi.

Amesema kuwa mwajili hatakiwi kumnyima ruhusa Katibu Mahsusi, kwani viongozi wakuu wa nchi wanatambua umuhimu wa makatibu hao katika kujenga maendeleo ya nchi kwani hakuna viongizi waliofanikiwa bila wao.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utumishi na Utawala bora wa Zanzibar, Seif Shaban Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itatoa ushirikiano wa dhati kujenga na kuongeza ushiriki wa Makatibu Mahsusi kwa maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Mahsusi nchini (TAPSEA), Zuhura Maganga amesema changamoto ya mtaala inarudisha nyuma taaluma yao ikiwa pamoja na kutokupandishwa madaraja kwa Makatibu Mahsusi jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya kada hiyo.
Waziri wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora, George Mkuchika akizungumza wakati akifungua rasmi Mkutano wa Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA), uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, jijini Arusha.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utumishi na Utawala bora wa Zanzibar, Seif Shaban Mwinyi akizungumza wakati akitoa salamu zake kwa wanachama wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA) wakati wa Mkutano wao Mkuu wa Mwaka, uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, jijini Arusha.
Mkuu wa Wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akizungumza wakati akitoa salamu zake kwa naiba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, katika Mkutano wa Mkuu wa Mwaka wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA), uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, jijini Arusha.
Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA), Zuhura Maganga akizungumza katika Mkutano wao Mkuu wa Mwaka, uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, jijini Arusha.
Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC), Seleman Shindika akizungumza katika Mkutano wao Mkuu wa Mwaka, uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa AICC, jijini Arusha.
Waziri wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora, George Mkuchika akipokea zawadi tuzo kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Makatibu Mahsusi Tanzania (TAPSEA), Zuhura Maganga.
Waziri wa Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala bora, George Mkuchika akimkabidhi tuzo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utumishi na Utawala bora wa Zanzibar, Seif Shaban Mwinyi.











































































































Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...