Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akiwa kwenye mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya Kusini mwa Afrika kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Norway, Bw. Germund Saether. Katika mazungumzo hayo, walijadili umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Norway hususan katika sekta za kukuza uchumi kwa maendeleo ya mataifa haya mawili. Mazungumzo hayo yamefanyika kwenye Ofisi ndogo za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki jijini Dar es Salaam tarehe 10 Mei 2019 
Kulia ni Balozi wa Norway hapa nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen pamoja na maafisa kutoka ubalozi huo wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Palamagamba John Kabudi na mgeni wake (hawapo pichani). 
Mazunguzmzo kati ya Mhe. Prof. Kabudi na Bw. Saether yakiendelea huku wajumbe wengine wakifuatilia. Pembeni kwa Mhe. Prof. Kabudi ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga pamoja na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo 
Picha ya pamoja 
Prof. Palamagamba John Kabudi akiagana na Mgeni wake. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...