Na Woinde Shizza Michuzi Tv, Arusha 
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro amewahakikishia mamia ya vijana waliojitokeza katika usahili wa kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kuwa usahili utafanyika kwa Uwazi na Ukweli na kusisitiza kuwa hapatakuwa na upendeleo zaidi ya kufuata Sheria pmoja na  sifa zinazotakiwa kwa vijana kujiunga na jeshi.
Aliyasema hayo leo ofisini kwakwe  wakati akiongea na Vijana waliojitokeza kwa wingi kuomba nafasi za kuingia katika mafunzo ya JKT ambapo kwa sasa usahili wa kuandikisha vijana hao kwa wilaya ya Arumeru unaendelea. 
DC Muro alibainisha kuwa wao kama watachagua vijana wote wenye sifa ya kujiunga na jeshi hilo na hawatamfumbia macho mtu yeyote ambaye atakuwa anawadanganya Vijana hao kuwa watoe ela ndio wapate nafasi 
"Wapo watu wanaopita uko barabarani wakiomba hela  huku wakiwa wanajinadi 
kwa kuwalaghai vijana hawa kuwa wanauwezo wakuwapa nafasi kitu ambacho sio chakweli hivyo kueni makini na msikubali kudanganywa mkatoa fedha zebu, nanapenda kusema ole wenu nyie tuwakute nyie walaghai hatua kali za kisheri tutawachukulia, na vijana iwapo mtu akiwafata kutaka fedha msisite kutoa taarifa sehemu husika"alisema DC Muro
Alifafanua kuwa zoezi hili la usahili linafanywa kwa uwazi na ukweli na katika zoezi hili hapatakuwa na upendeleo wowote ule Kwani sheria zitafutwa. 
Aidha alibainisha mara baada ya kukamilisha uchambuaji wa majina kwa vigezo vya sifa na nafasi zilizopo watabandika majina kwa vijana watakaopita awamu ya kwanza na kisha kuingia awamu ya pili ya vipimo vya kubaini afya za vijana kikiwemo kipimo cha madawa ya kulevya pamoja na bangi.
Aliwapongeza vijana wote waliojitokeza kujiunga na jeshi lakujenga taifa (JKT) Na kubainisha kuwa wametaka kumuunga mkono Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwa kufanya kazi kwa uweledi ,ukweli na uwaminifu. 
"Vijana hawa wamejitokeza kwa wingi na hii wameonyesha dhamiranzuri yakutaka kutumikia taifa lao kupitia jeshi la ulinzi na usalama nanapenda kuwapongeza sana kwani wameuonyesha uzalendo mzuri wa kutaka kutumikia taifa lao "alisema Muro. 
Alisema kuwa wanaamini kuwa unapokuwa na jeshi imara najeshi lenye nithamu ,basi hilo ndio jeshi sahii kwaajili ya Kupambana ,  Kulinda nakupigania taifa letu .
Mkuu Wilaya ya Arumeru  Mhe. Jerry Muro akiongea navijana waliojitokeza ofisini kwakwe kwa ajili wa usahili wa kuingia Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...