Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akisalimiana na kamishna wa Operesheni na Mafunzo CP Liberatus Sabas, wakati alipowasili katika viwanja vya Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuzungumza na Maofisa na Wakaguzi wa Jeshi hilo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akimsikiliza Mkuu wa Utawala wa Jeshi la Polisi DCP Lucas Mkondya (aliyesimama) wakati akitoa hotuba mbele ya maofisa na wakaguzi (hawapo Pichani) kwenye kikao cha kuwajengea uwezo wa kiutendaji na kuwakumbusha wajibu wao.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na makamishna wa jeshi hilo baada ya kumaliza mkutano uliowahusisha maofisa na wakaguzi kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiutendaji, kutoka kulia kwake ni Kamishna wa kamisheni ya Ushirikishwaji wa Jamii CP Mussa A. Mussa na kushoto kwake ni Kamishna wa Operesheni na Mafunzo CP Liberatus Sabas. (Picha na Jeshi la Polisi).
|
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...