Mkuu
wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, amewataka Maofisa na askari kuhakikisha
wanaendelea kutimiza wajibu wao kikamilifu na kutokujiingiza kwenye masuala ya
uhalifu ikiwemo kushiriki kwenye wizi wa dhahabu sambamba na uhujum uchumi.
IGP
Sirro, ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam, wakati alipokuwa akizungumza na
Maofisa na Wakaguzi wa Jeshi hilo ambapo amesema kuwa, hatua kali za kisheria
zitachukuliwa kwa askari anayeshiriki kwenye uhalifu ikiwemo kufukuzwa kazi
pamojana kufikishwa mahakamani.
Hata
hivyo IGP Sirro amesema Jeshi la Polisi limejipanga kikamilifu katika
kuhakikisha suala la uchaguzi linafanyika kwa amani na utulivu na kwamba amewahakikishia
wananchi usalama wao na mali zao na kuwataka wananchi kuendelea kushirikiana na
Polisi kwa kutoa taarifa sahihi za uhalifu na wahalifu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...