Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto, Mhandisi Jairos Nkoroka (wa tatu kulia) pamoja na wafanyakazi wakikagua propella za vivuko vilivyohifadhiwa katika karakana ya mji wa Ifakara baada ya daraja la mto Kilombero kukamililika. Vivuko hivyo, MV.Kilombero I na II vitaanza kukarabatiwa na kuunganishwa hivi karibuni tayari kwa hatua ya kupelekwa katika eneo la Kikove Malinyi kwa ajili ya kutoa huduma. 
 Mhandisi Jairos Nkoroka kushoto akimuonyesha Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle mashine ya kugandamiza vipuri vya magari (press machine) wakati alipotembelea kukagua utendaji kazi wa karakana hiyo mpya ya TEMESA iliyoanza kutoa huduma mwezi Juni mwaka huu katika Halmashauri ya mji wa Ifakara wilayani Kilombero mkoani Morogoro. Karakana hiyo sasa itahudumia wilaya zote za karibu ikiwemo wilaya ya Ulanga na Malinyi ambazo awali zilikuwa zikitegemea kupata huduma Morogoro mjini.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua mashine ya kupimia uwiano wa matairi ya magari (wheel balance) iliyopo katika karakana ya TEMESA katika Halmashauri ya mji wa Ifakara wakati alipoitembelea kujionea utendaji kazi wake mara baada ya kuanza kutoa huduma Juni mosi mwaka huu. Karakana hiyo sasa itahudumia wilaya zote za karibu ikiwemo wilaya ya Ulanga na Malinyi ambazo awali zilikuwa zikitegemea kupata huduma za matengenezo ya magari na mitambo kutoka Morogoro mjini.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle (wa pili kushoto) akifurahia jambo na wafanyakazi mara baada ya kumaliza kukagua mipaka ya karakana ya TEMESA Ifakara iliyoanza kutoa huduma Juni mosi mwaka huu katika Halmashauri ya mji wa Ifakara wilayani Kilombero mkoani Morogoro. Karakana hiyo sasa itahudumia wilaya zote za karibu ikiwemo wilaya ya Ulanga na Malinyi ambazo awali zilikuwa zikitegemea kupata huduma za matengenezo ya magari na mitambo kutoka Morogoro mjini.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kulia akikagua kivuko cha MV. Kilombero I kilichohifadhiwa katika karakana ya mji wa Ifakara baada ya daraja la mto Kilombero kukamililika. Kivuko hicho pamoja na kivuko cha MV. Kilombero II vitaanza kukarabatiwa na kuunganishwa hivi karibuni tayari kwa hatua ya kupelekwa katika eneo la Kikove Malinyi kwa ajili ya kutoa huduma.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle kushoto akikagua kivuko cha MV Kilombero II ambacho kimehifadhiwa katika karakana hiyo baada ya huduma za kivuko kufungwa katika mto Kilombero kutokana na kukamilika kwa daraja. Kivuko hicho pamoja na kivuko cha MV. Kilombero I vinatarajiwa kuanza kufanyiwa ukarabati tayari kwa hatua ya kupelekwa katika eneo la Kikove Malinyi kwa ajili ya kutoa huduma katika maeneo hayo.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Japhet Y. Maselle katikati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa karakana mpya ya TEMESA iliyopo katika Halmashauri ya mji wa Ifakara wilayani Kilombero mara baada ya kumaliza kukagua karakana hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...