Na Veronica Kazimoto
Naibu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Msafiri Mbibo
ametembelea bandari kavu ya Said Bakhresa (SSB-ICD) na African ICD
ambapo amewataka Maofisa Forodha wa Mamlaka hiyo kuzingatia uwajibikaji,
weledi na uadilifu wakati wote wanapotimiza majukumu yao ya kila siku.
Akizungumza
na maofisa hao kabla ya kukagua mizigo iliyopo katika bandari hizo,
Naibu Kamishna Mkuu huyo amesema kwamba, uzingatiaji wa maadili katika
sehemu za kazi utasaidia kuondoa malalamiko na kero kwa walipakodi ambao
ni wadau wakuu wa TRA.
“Jukumu
la kujenga taswira ya mamlaka ni la kila mtumishi wa TRA. Hivyo, ni
wajibu wa kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anafanya kazi bila upendeleo,
anawajali wateja ikiwa ni pamoja na kutumia lugha yenye staha, alisema
Naibu Kaimshna Mkuu Mbibo.
Kwa
upande wake Kamishna wa Forodha na Ushuru wa Bidhaa, Ben Usaje
amewasisitiza watumishi hao kutojihusisha na vitendo vya rushwa ambavyo
vinaichafua Mamlaka ya Mapato Tanzania.
“Sote
humu ndani tunajua kuwa, kupokea au kutoa rushwa ni kinyume cha sheria
ya nchi yetu na yeyote atakayebainika akifanya hivyo atachukuliwa hatua
kwa mujibu wa sheria. Hivyo, hakikisheni mnaepuka kabisa vitendo hivyo
vya rushwa kwani vitawasababishia kupoteza kazi na kufikishwa
mahakamani”, alisema Usaje.
Baadhi
ya majukumu ya Ofisi za Forodha zilizopo katika bandari kavu hapa
nchini ni kuhakikisha kuwa taratibu zote za kuingiza mizigo ndani ya
nchi zinafuatwa pamoja na kuhakikisha kwamba kodi stahiki inalipwa na
wenye mizigo kabla ya kutoa mizigo yao katika bandari hizo.
Meneja
wa Bandari Kavu ya African ICD, Abeid Said (wa kwanza kulia) akitoa
maelezo kuhusu bandari hiyo kwa Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) Msafiri Mbibo (wa pili kushoto aliyevaa tai ya mistali)
wakati alipotembelea bandarini hapo.
Afisa
Forodha Mfawidhi wa Bandari Kavu ya African ICD, Brian Japheth akitoa
maelezo juu ya mizigo iliyopo bandarini hapo kwa Naibu Kamishna Mkuu wa
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Msafiri Mbibo (wa pili kulia) wakati
alipoitembelea bandari hiyo. Kushoto kwake ni Kamishna wa Forodha na
Ushuru wa Bidhaa, Ben Usaje.
Afisa
Forodha Mfawidhi wa Bandari Kavu ya Said Bakhresa (SSB-ICD), Caleb
Mwangalaba akitoa maelezo mafupi kuhusu bandari hiyo kwa Naibu Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Msafiri Mbibo (kushoto) wakati
alipoitembelea bandari hiyo kuona jinsi inavyofanya kazi.
Naibu
Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Msafiri Mbibo
(aliyevaa tai ya mistali) akiwa katika picha ya pamoja na Maofisa wa
Forodha waliopo katika bandari kavu ya African ICD wakati alipoitembelea
bandari hiyo. Kushoto kwa Naibu Kamishna Mkuu ni Kamishna wa Forodha na
Ushuru wa Bidhaa, Ben Usaje na kulia kwake ni Naibu Kamishna wa
Biashara na Uwezeshaji, Godfrey Kitundu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...