* ACHANGIWA MILIONI 13 NA AKO GROUP NA CHAMA CHA WASHEHERESHAJI.

Kampeni ya Matibabu ya upasuaji wa moyo kwa watoto 60 kutoka familia zenye maisha duni iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda imezidi kugusa Mioyo ya wadau na watu mbalimbali ambapo leo Kampuni ya Ako Group Ltd imeahidi kutoa mchango Shilingi Milioni10 kwaajili ya matibabu ya watoto 5 huku wanachama wa Chama cha Washehereshaji Tanzania wakichangia kiasi Cha Shilingi milioni 3.3 kwaajili ya matibabu kwa watoto wenye tatizo la moyo.

RC Makonda amesema fedha hizo zitawezesha matibabu ya upasuaji wa moyo kwa Watoto 7 ambapo ametoa wito kwa wadau, taasisi na kampuni mbalimbali kusaidia matibabu ili kuokoa maisha yao.

Hayo yamejiri wakati wa mkutano mkuu wa Chama cha Washehereshaji ambapo katika michango hiyo kampuni ya Ako Group Ltd imetoa ahadi ya kusaidia matibabu ya watoto 5 na chama cha washehereshaji kimejitolea kugharamia matibabu kwa watoto 2 na kufanya idadi kuwa watoto7.

Itakumbukwa jumamosi ya juni 22 RC Makonda alitoa ufadhili wa matibabu ya upasuaji wa moyo kwa watoto 10 kati ya 60 ikiwa ni mkakati wake wa matibabu ya watoto 10 kila mwezi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...