Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akijibu swali bungeni leo tarehe 10 Juni 2019 wakati wa mkutano wa kumi na tano wa Bunge la Bajeti Jijini Dodoma. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo).
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) akijibu swali bungeni leo tarehe 10 Juni 2019 wakati wa mkutano wa kumi na tano wa Bunge la Bajeti Jijini Dodoma. 

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Serikali imearifu kuwa inafanya utafiti na tathmini ya kina ya maji kujaa kwenye mashamba ya wakulima katika maeneo mbalimbali nchini.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 10 Juni 2019 wakati akijibu swali la Mhe Yahaya Omary Massare wa Jimbo la Manyoni Magharibi aliyetaka kufahamu serikali ina mpango gani kuwasaidia wananchi kwa kuwajengea mifereji ya kuongoza maji yasiingie mashambani.

Mbunge huyo alisema kuwa Eneo la Mbuga linalozunguka Mji wa Itigi pamoja na kufaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali kama Mahindi, Alizeti, Choroko na Dengu lakini eneo hili linajaa maji na kufanya kilimo kuwa kigumu.

Mhe Mgumba aliongeza kuwa Utafiti na tathmini hiyo itakapokamilika itakuja na mikakati na mapendekezo stahiki yatakayosaidia kutatua changamoto ya kujaa maji mashambani na kuwasaidia  wakulima wa eneo la mbuga linalozunguka mji wa Itigi ili kuongeza uzalishaji na tija.

Aliongeza kuwa eneo la mbuga linalozunguka mji wa Itigi limekuwa likijaa maji pale mvua zinapokuwa juu ya wastani ambapo historia inaonesha kuwa bonde hili lilijaa maji kipindi cha mwaka 1997/1998 wakati wa mvua za E-lnino na katika msimu wa 2015/2016 baada ya miaka tisa tangu wakati wa mvua za E-lnino mwaka 1997/98.

Aidha, alisema kuwa Serikali imelichukua suala la Mheshimiwa Mbunge na itatuma wataalam wa Kilimo na Tume ya Umwagiliaji kwa ajili ya kwenda kufanya utafiti na tathmini ya kina ya maji kujaa kwenye mashamba ya wakulima.

Utafiti na tathmini hiyo itakapokamilika itakuja na mikakati na mapendekezo stahiki yatakayosaidia kutatua changamoto ya kujaa maji mashambani na kuwasaidia  wakulima wa eneo la mbuga linalozunguka mji wa Itigi ili kuongeza uzalishaji na tija.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...