Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akizungumza jambo wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha Kujadili Mpango Kabambe wa Jiji la Dodoma, kuhusu mpango wa michoro ya Majengo ya Wizara Awamu ya Pili katika Mji wa Serikali na Michoro ya Miundombinu ya Chini ya Ardhi walipokutana na kikosi kazi cha kuratibu zoezi la Serikali kuhamia Dodoma hii leo Juni 20, 2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa ofisi hiyo Jijini Dodoma.
 Sehemu ya wajumbe wa mkutano huo wakifuatilia neno la ufunguzi kutoka Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi (hayupo pichani).
 Baadhi ya wajumbe wakikao hicho wakifuatilia neno la ufunguzi kutoka Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi (hayupo pichani) walipokutana kujadili masuala ya mpango Kabambe wa Jiji la Dodoma ikiwa ni sehemu ya uratibu wa zoezi la Serikali kuhamia Dodoma.
 Mwenyekiti wa Timu ya Kutengeneza Mpango Kabambe wa Jiji la Dodoma Prof. John Lupala akichangia jambo wakati wa kikao hicho.
 Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge na Waziri Mkuu) Bi. Maimuna Tarishi akifuatilia michango ya wajumbe walioshiriki katika kikao kazi cha Kujadili Mpango Kabambe wa Jiji la Dodoma, kuhusu mpango wa michoro ya Majengo ya Wizara Awamu ya Pili katika Mji wa Serikali na Michoro ya Miundombinu ya Chini ya Ardhi walipokutana na kikosi kazi cha kuratibu zoezi la Serikali kuhamia Dodoma hii leo Juni 20, 2019.
Baadhi ya wajumbe wa kikao kazi cha Kujadili Mpango Kabambe wa Jiji la Dodoma, kuhusu mpango wa michoro ya Majengo ya Wizara Awamu ya Pili katika Mji wa Serikali na Michoro ya Miundombinu ya Chini ya Ardhi walipokutana na kikosi kazi cha kuratibu zoezi la Serikali kuhamia Dodoma Juni 20, 2019.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...